• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC RUVUMA atahadharisha shughuli za kiuchumi zisizozingatia sheria na kanuni

Imewekwa kuanzia tarehe: May 19th, 2024

Na Albano Midelo,Songea

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed ametahadharisha kuwa shughuli za kiuchumi zisipofanywa kwa kuzingatia ushauri wa kitaalam zinaweza kuharibu mazingira na kutishia mustakabali wa Maisha ya viumbehai.

Kanali Abbas ametoa tahadhari hiyo wakati anazungumza kwenye maadhimisho ya siku ya Uhuru wa vyombo vya Habari Duniani ambazo kimkoa zimefanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea na  kuhudhuriwa na wadau wa Habari na na wanahabari.

“Kuna uchimbaji wa madini unafanyika kwa mtazamo ni shughuli ya kiuchumi kama isipofanywa vizuri kwa kuzingatia sheria,kanuni na ushauri wa kitalaam,unaweza kugeuka uchumi wenye kuharibu mustakabari wa maisha ya watu’’,alisisitiza.

Amesema kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu inayosema uandishi wa Habari  na changamoto za mabadiliko ya tabia nchi,inakwenda kuugusa muhimili wa Habari ili  wanahabari wakafanye kazi ya kuhabarisha umma  kuhusu madhara yanayoweza  kutokea kwa kutozingatia kanuni na sheria  za uendeshaji wa shughuli za kiuchumi hivyo kusababisha mabadiliko ya tabianchi na  hali ya hewa.

Amesema Rais Dkt.Samia amefanya kazi kubwa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ambapo ameweza kuanzisha mikakati na program mbalimbali ili kuhakikisha taifa na Dunia inaendelea kuwa salama kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Amebainisha kuwa hivi karibuni Rais  Samia amezindua  mkakati wa nishati safi ikiwa ni sehemu ya uendelezaji wa kampeni  za kupambana na mabadiliko ya tabianchi na  hali ya hewa.

Amesema madhara yameanza kujitokeza ambapo hivi sasa kumekuwa  na ongezeko kubwa la joto kwenye uso wa dunia,pia kumekuwa na uyeyushaji wa  barafu kwenye bahari na kusababisha ongezeko la maji ambalo pia limesababisha madhara mengi ikiwemo elnino na lanina.

Ameongeza kuwa kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa kumetokea madhara mbalimbali kama vimbunga ambapo hivi karibuni kimetokea kimbunga Hidaya  ambacho kimeleta madhara makubwa.

Amesema madhara ya mabadiliko ya tabianchi ni mengi na kwamba yasipoelezwa vizuri kwa wananchi kupitia vyombo mbalimbali vya habari, wananchi wanaweza kuendelea kufanya shughuli za kiuchumi  bila kufuata kanuni na sheria,hivyo amesisitiza kuyatunza mazingira ili Taifa liendelee kuwa salama.

Akizungumzia maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya Habari Duniani,Kanali Abbas amewapongeza wanahabari kwa kufanya kazi nzuri ya kuhabarisha umma kazi mbalimbali zinazofanyika na serikali ndani ya Mkoa wa Ruvuma na Taifa kwa ujumla.

Hata hivyo ametahadharisha kuwa wakati wanahabari wanatekeleza majukumu yao,wasiache kuangalia utekelezaji wa 4R za Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Ameahidi serikali ya Mkoa wa Ruvuma ipo tayari kushirikiana na wanahabari na kwamba yupo tayari kutoa kila aina ya ushirikiano unaohitajika ili kuhakikisha kazi ya wanahabari  inakuwa nyepesi na matakwa ya muhimili wa kuhabarisha umma haukwami.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Songea Mheshimiwa Kapenjama Ndile  amesema  katika Tanzania sheria zinawapa heshima kubwa waandishi wa Habari na kwamba Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazoheshimu uhuru wa Habari.

Ndile amesisitiza kuwa huwezi kuheshimu vyombo vya Habari bila kuheshimu wanahabari wenyewe  ambapo amesema wanahabari wamefanyakazi kubwa iliyotuka katika wilaya ya Songea na Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Ruvuma Amon Mtega amempongeza  Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kwa kuyaunganisha makundi mbalimbali wakiwemo wanahabari .

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.