• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC Ruvuma atoa maagizo ya mwaka mpya wa masomo

Imewekwa kuanzia tarehe: January 14th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, amewataka wasimamizi wa elimu ngazi ya mkoa, wilaya na halmashauri kuhakikisha watoto wenye umri wa kwenda shule wanaandikishwa na waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wanaripoti shuleni.

Ameyasema hayo wakati akifanya mkutano na waandishi wa habari kuhusu mwaka mpya wa masomo, uliofanyika katika ofisi yake iliyopo mjini Songea mkoani Ruvuma.

"Tuendeleze kasi na nguvu ya kusimamia zoezi hili ili liwe na mafanikio makubwa, kila mtoto anayestahili kandikishwa awe ameandikishwa, wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wahakikishe wote wanaripoti shule, viongozi waliopo katika mamlaka ya ngazi za wilaya na halmashauri wahakikishe wanaendelea kusimamia zoezi hilo ili wale ambao wanakiuka sheria wachukuliwe hatua,"alisema Kanali Ahmed.

Ameongeza kuwa zoezi hilo liende sawa na kuhakikisha wazazi wanawapatia watoto wao mahitaji stahiki ikiwemo sare za shule, shajara na kuhakikisha mtoto anapata chakula shuleni ili kumpunguzia vikwazo katika masomo yake.

Amemsisitiza kila mdau anayehusika na ujenzi wa miundombinu ya shule kuhakikisha anatimiza wajibu wake, miradi ya ujenzi inayojegwa izingatie ufanisi pamoja na kukamilishwa mapema ili wanafunzi waweze kuitumia miundombinu hiyo.

Kwa upande mwingine ameiagiza Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa na Halmashauri kuchukua hatua za kinidhamu kwa mtu yoyote anayerudisha nyuma usimamizi wa elimu katika mkoa, hivyo kusiwe na vikwazo vyovyote vya kumpokea wanafunzi shuleni kwa kisingizio chochote cha mzazi kutotimiza mahitaji ya shule kwa sababu ni muhimu kila mwanafunzi kuanza masomo na wenzake kwa wakati.

Pia, ametoa maelekezo kwa walimu wote kuhakikisha wanahudhuria darasani na kufundisha wanafunzi kama taratibu za kazi yao inavyowataka, malezi kwa kipindi chote wanafunzi wanapokuwa shuleni, kusimamia upandaji wa miti ya matunda kwaajili ya kujenga na kulinda afya za wanafunzi na kuhakikisha kila shule inakuwa na bustani za mbogamboga na shamba la mazao ya chakula lisilopungua hekari tatu.

Katika hatua nyingine, ametembelea Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songea (Songea Girls) na Sekondari ya Mfaranyaki kujionea hali ilivyo, ambapo amewasisitiza wazazi kuhakikisha wanajitolea kwa hali na mali ili kufanikisha suala la elimu, maafisa elimu kata kuwa wasimamizi wa awali, wasimamizi wa elimu ngazi ya msingi na sekondari pamoja na wadhibiti ubora kuhakikisha wanakuwa karibu na shule ili ubora wa elimu unaokusudiwa upatikane.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.