• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC RUVUMA awaagiza maafisa elimu kuinua ufaulu

Imewekwa kuanzia tarehe: February 19th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, amewataka maafisa elimu kata wa Mkoa wa Ruvuma kujipanga upya na  kutimiza wajibu wao ili kuondokana na changamoto za kutofanya vizuri kitaaluma.

Ametoa rai hiyo wakati akihitimisha mkutano wa tathmini wa maafisa elimu kata Mkoa wa Ruvuma, uliofanyika katika ukumbi wa kanisa la Anglican manispaa ya Songea.

Amewasisitiza kuwa wabunifu kutatua matatizo badala ya kulalamika, kuwasimamia walimu wafanye kazi na kutoa taarifa iwapo hawafanyi kazi ipasavyo,  kuongeza kasi ya kusimamia wanafunzi kumudu stadi za KK kabla ya darasa la tatu, kuhakikisha mada zinakamilika na kupata muda wa marudio, na kuhakikisha kata zao zinafaulisha kwa asilimia zisizopungua 50 kwa daraja la kwanza hadi la tatu kwa mitihani ya kidato cha nne.

Kanali Ahmed amesema katika mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi kwa mwaka 2024 mkoa wa Ruvuma umefaulisha kwa asilimia 69.34  ambapo ufaulu umepanda kwa asilimia 0.28 kutoka ufaulu wa asilimia 69.06 kwa mwaka 2023, kwa darasa la nne ufauli ni asilimia 77 ukipanda kwa asilimia 1.76 kutoka ufaulu wa asilimia 76.01 

Hata hivyo amesema  kwa upande wa kidato cha pili na cha nne mwaka 2024 bado ufaulu sio mzuri, amesema ufaulu wa kidato cha pili ni asilimia  82.34 ambapo asilimia 17.66 ya wanafunzi wamebaki kidato cha pili ambao wengi huacha shule na kutofikia ndoto zao,  ufaulu wa kidato cha nne ni  asilimia 92.39 huku wenye daraja la kwanza hadi la tatu hawakufikia asilimia 50

Afisa Elimu Mkoa wa Ruvuma, Mwalimu Edith Mpinzile, amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kufanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya elimu.

Ameeleza kuwa, serikali inaboresha miundombinu ya ufundishaji na ujifunzaji, kutoa fedha za uendeshaji wa shule, kulipa malimbikizo ya madeni, na kupandisha vyeo vya walimu, huku ikiendelea kusikiliza na kutatua kero za walimu na kuboresha hadhi ya walimu ili kuhakikisha Elimu inatoa matokeo bora.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.