• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC RUVUMA aagiza kukamilishwa ujenzi vituo vya afya Lilambo na Mletele

Imewekwa kuanzia tarehe: November 28th, 2022

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kukamilisha ujenzi wa vituo vya afya Lilambo na Mletele ili vianze kuwahudumia wananchi.

Kanali Thomas ametoa maagizo hayo baada ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo.

Amesema kumekuwa na changamoto ya umaliziaji wa miradi hivyo ameuagiza uongozi wa Manispaa ya Songea kutoa fedha za kumalizia vituo vya afya.

Amesema serikali inaendelea kutoa mabilioni ya fedha kutekeleza miradi mbalimbali  ambapo Serikali kupitia mapato ya ndani katika Manispaa ya Songea imetoa shilingi milioni  514 kutekeleza ujenzi Kituo cha Afya Lilambo na zaidi ya shilingi milioni 545 zimetolewa na serikali Kuu kupitia Global Fund kutekeleza ujenzi kituo cha afya Mletele.

“Nichukue fursa hii kuwapongeza Manispaa ya Songea kwa kusimamia ujenzi wa kituo cha Afya Lilambo ambacho kinatumia mapato ya ndani ,hata hivyo ongezeni kasi ili mkamilishe ujenzi wa Kituo hiki ulioanza mwaka jana “,alisisitiza RC Thomas. 

Mkuu wa Mkoa pia amekagua ujenzi wa madarasa 14 kati ya 76 yanayojengwa katika shule za sekondari Manispaa ya Songea kwa gharama ya shilingi bilioni 1.5.

Ameagiza ujenzi wa madarasa hayo na samani zake kukamilika kama ilivyopangwa kwa kuzingatia viwango ili yaanze kutumika Januari 2023.

Amewaagiza wakuu wa Wilaya kujenga utamaduni wa kukagua mara kwa mara miradi yote ya maendeleo ambayo serikali inatoa fedha.

Akitoa taarifa ya miradi hiyo kwa Mkuu wa Mkoa,Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Dkt.Federick Sagamiko amesema katika kipindi cha Julai 2021 hadi Oktoba 2022,Manispaa hiyo imepokea shilingi bilioni 2.7 toka serikalini kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali katika sekta za elimu,afya,Utawala na Maendeleo ya Jamii.

Mkuu wa Wilaya ya Songea Mheshimiwa Pololet Mgema amesema licha ya changamoto zilizopo ujenzi wa madarasa 96 katika Wilaya hiyo unaendelea vizuri na wanatarajia kumkabidhi madarasa hayo Mkuu wa Mkoa Desemba 10 mwaka huu.

Amewaagiza waandisi wanaosimamia miradi kuwa kwenye miradi wakati wote ili itekelezwe kwa viwango.Ameahidi dosari zote zilizojitongeza kwenye ukaguzi kufanyiwa kazi haraka.

Wilaya ya Songea inaundwa na Halmashauri tatu za Halmashauri ya Manispaa ya Songea, Halmashauri ya Madaba na Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma 

Novemba 28,2022.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.