• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC THOMAS ahimiza wananchi kushiriki sensa ya watu na makazi

Imewekwa kuanzia tarehe: August 21st, 2022

MKUU wa mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas,amewataka wananchi wa mkoa huo kuhakikisha wanashiriki vyema zoezi la sensa ya watu na makazi  ili kuisaidia serikali kupata takwimu sahihi pale inapotaka kupanga mipango ya maendeleo kwa wananchi wake.

Kanali Thomas ametoa wito huo jana wakati akizungumza na wananchi na viongozi wa wilaya Namtumbo,akiwa katika ziara ya kuhamasisha wananchi  kujiandaa kushiriki zoezi hilo linalotarajiwa kufanyika tarehe 23 wiki ijayo.

Amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa makarani wa sensa na kuhakikisha watu wenye ulemavu,watoto na wanawake wanakuwa mstari wa mbele na kujitokeza kuhesabiwa na kamwe wasijaribu kuwaficha majumbani kwa kuwa ni kosa na hawatawatendea haki.

Katika hatua nyingine mkuu wa mkoa,amewakumbusha wananchi  juu ya suala la kujiwekea akiba ya chakula    kama  tahadhari ya kutokea na kupatwa na tatizo la njaa katika familia zao.

Alisema hali ya uzalishaji katika msimu wa kilimo 2021/2022 haukuwa mkubwa,kutokana na changamoto ya upatikanaji wa pembejeo kwa baadhi ya wakulima,hata hivyo kiasi cha chakula kilichozalishwa ni lazima kitunzwe.

Alisema,kufuatia wimbi kubwa la wafanyabiashara kutoka mikoa mingine  na nchi jirani walioingia kwa wingi kwa ajili ya kununua mahindi ni dhahiri kuwa chakula kilichozalishwa msimu 2021/2022  hakitatosheleza,hivyo ni muhimu wananchi kuchukua tahadhari  hiyo badala ya kuuza chakula chote kutokana na tamaa ya fedha.

Aidha Kanali Laban, amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuondoa ruzuku kwenye pembejeo ambapo bei ya mbolea katika msimu wa kilimo 2022/2023 itashuka kutoka Shilingi 120,000 hadi  shilingi 70,000 kwa mfuko mmoja.

Alisema, hayo ni mafanikio makubwa kwa serikali hasa ikizingatiwa kuwa,wananchi  wa mkoa wa Ruvuma wanategemea  shughuli za kilimo kwa ajili ya kuendesha maisha yao ya kila siku.

Kanali Laban,amewaonya watendaji wa serikali watakaosimamia ugawaji wa pembejeo hizo kuepuka upendeleo na kutojihusisha na vitendo vya rushwa wakati wa zoezi la ujazaji wa fomu kwa ajili ya kuwatambua wakulima.

Naye Waziri wa nchi ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora Jenista Mhagama amewaomba Watanzania kuendelea kumuombea Rais  Samia Suluhu Hassan ili aweze kutekeleza majukumu yake vizuri.

Alisema,licha ya matatizo  vita kati ya Ukraine na Urusi iliyosababisha kupanda kwa baadhi ya bidhaa na  gharama ya maisha,lakini  Rais Samia anafanya kazi kubwa ya kutatua changamoto mbalimbali kwa wananchi ikiwamo kuendelea kutoa fedha kwa kaya maskini na kuondoa ruzuku kwenye mbolea.

Mhagama,amewaomba wakulima kutumia muda wao kwenye shughuli za kilimo ili kuongeza uzalishaji wa chakula mashambani kwa kuwa, mazao ya chakula hususani zao la mahindi limekuwa zao kubwa la biashara.

Diwani wa kata ya Luchili Othman Njovu alisema,wananchi wa kata hiyo wataendelea kushirikiana na serikali katika shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwamo zoezi la sensa ya watu na makazi.

Njovu amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zao katika kuwatumikia wananchi na kuondoa ruzuku kwenye pembejeo za kilimo ambapo alieleza kuwa,hatua hiyo itaongeza uzalishaji wa mazao katika msimu wa kilimo 2022/2023.

“wananchi wa kata ya Luchili wamejiandaa  na wako tayari kwa ajili ya kuhesabiwa siku ya tarehe 23 mwezi huu,hatutaki kuiangusha serikali yetu kwenye mambo muhimu ya maendeleo”alisema Njovu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.