• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RTO RUVUMA awataka madereva wa mabasi makubwa kuzingatia sheria

Imewekwa kuanzia tarehe: June 23rd, 2022

MKUU wa kikosi cha Usalama Barabarani mkoani Ruvuma Salum Morimori,amewataka madereva kutii,  kuzingatia sheria na alama za usalama Barabarani kama zinavyoelekeza ili kuepuka ajali ambazo hupelekea watu kupoteza maisha au kuwasababishia ulemavu wa kudumu.

Morimori ametoa kauli hiyo jana, alipokuwa akizungumza na madereva wa mabasi yaendayo mikoani baada ya kufanya ukaguzi wa kustukiza katika kituo kikuu cha mabasi mjini Tunduru.

Alisema, baadhi ya madereva wa mabasi hawataki kuzingatia sheria na kufuata alama za barabarani na kutoa onyo kwa madereva wazembe kuwa, Jeshi la Polisi litawachukulia hatua kali ikiwamo kuwafikisha mahakamani  wale wote wasiotaka kuzingatia au kufuata sheria zilizopo.

Alisema,kumekuwa na tabia ya madereva wa vyombo vya moto hasa mabasi ya abiria kuvunje sheria za usalama barabarani kwa makusudi na kusababisha ajali huku wakiwa wanazitambua sheria hizo.

“unakuta dereva anajua kabisa kwamba anavunja sheria za usalama barabarani  lakini anaendelea kwa makusudi, tabia hii inachangia sana kuongezeka kwa ajali,natoa rai kwa madereva na wananchi wa mkoa wa Ruvuma kuhakikisha wanafuata na kuzingatia sheria hizo za barabarani”alisema Afande Morimori.

Kwa mujibu wa Morimori,kumekuwa na matumizi na tabia mbaya ya alama kama vile kupita kwa mwendo kasi zaidi ya spidi hamsini(50)kwenye makazi ya watu na kwenye vivuko(Zebra).

“kuna madereva wanaovuta bangi na kunywa pombe,watu kama hao tutawashughulikia kwa kuwawka maabusu na kuwafikisha mahakamani,Ruvuma hatutaki madereva wazembe huu ni mkoa salama”alisema.

Alisema,wakati mwingine madereva kuongea na simu bila kujali usalama wa watumiaji wengine wa barabara hizo, na kuwaomba wananchi wakiona dereva anaongea na simu au kuendesha gari kwa mwendo kasi ni vyema kutoa taarifa kwa Askari wa usalama barabarani.

Alisema, sio vizuri na wala haikubariki  kisheria kwa abiria kuwa sehemu ya tatizo kwa kufurahia mwendo kasi  wa dereva ambao  unaweza kuhatarisha maisha yao, badala yake kulisaidia Jeshi  hilo  kuwafichua madereva wasiotaka kuzingatia sheria hizo.

Amewaomba wananchi wa mkoa wa Ruvuma,kuendelea kuzingatia na kufuata sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali ambazo zimekuwa chanzo cha kupoteza maisha ya watu wengi na nguvu kazi ya Taifa.

Katika ukaguzi huo ulioongozwa na Mkuu huyo wa kikosi cha usalama mkoa kwa kushirikiana na askari wa usalama barabarani wilayani Tunduru, baadhi ya magari  yalikutwa na makosa mbalimbali ikiwamo matairi kuwa na vipara na madereva kuendesha kwa mwendo kasi ambapo wale waliokutwa na makosa hayo waliandikiwa faini na kutakiwa kufanya marekebisho ya kasoro hizo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.