• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RUVUMA wamshukuru Rais kwa fedha za ujenzi wa sekondari mpya za kisasa

Imewekwa kuanzia tarehe: February 9th, 2023

WANANCHI mkoani Ruvuma wamemshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu kwa kutoa fedha ambazo zimewezesha kujengwa kwa sekondari mpya zenye mazingira ya kuvutia katika Halmashauri zote nane.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga Grace Quietine amesema Rais ametoa shilingi milioni 470 kujenga sekondari mpya katika Kata ya Lusonga ambayo imekamilika kwa zaidi ya asilimia 90.

Amesema kiasi hicho cha fedha kimewezesha kujenga jengo la utawala,vyumba nane vya madarasa,maabara tatu,jengo la TEHAMA,jengo la maktaba,vyoo matundu 20 na  sehemu ya kunawia  maji mikono wanafunzi.

Amesema tayari wanafunzi wa kidato cha kwanza wamesajiriwa na kuanza masomo ambapo hivi sasa shughuli za umaliziaji zinaendelea zikiwemo za kuweka mfumo wa gesi na maji katika majengo ya maktaba na kwamba Halmashauri pia imeongeza fedha za kukamilisha mradi huo ambapo hadi sasa zaidi ya shilingi milioni 492 zimetumika.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru Chiza Marando  amesema anamshukuru Rais kwa upendeleo wa pekee wa kuwapatia kiasi cha shilingi bilioni 1.4 kujenga sekondari mpya tatu za mfano katika wilaya hiyo ambazo zimekamilika na kuanza kuchukua wanafunzi wa kidato cha kwanza.

Amesema kila sekondari imepewa shilingi milioni 470 na kuzitaja sekondari hizo kuwa zimejengwa katika kata za Nakayaya,Majimaji na Lukumbule na kwamba kila shule imejenga jengo la utawala,madarasa nane,vyoo,samani,maabara tatu,jengo la TEHAMA na maktaba.

“Shule zote tatu zinaendelea na hatua za ukamilishaji,lakini tumeshazisajiri na tumeshazifungua,wanafunzi wanaendelea kusoma, tunamshukuru sana Rais kwa kutumbuka Tunduru’’;alisema Marando.

Hata hivyo amesema kufunguliwa kwa shule hizo kumepunguza kero ya wanafunzi kwenye kata hizo kusafiri umbali mrefu kufuata sekondari.

Rais Samia pia ametoa shilingi milioni 470 kujenga sekondari mpya katika Kata ya Msisima Halmashauri ya Namtumbo na kwamba sekondari hiyo imefunguliwa na wanafunzi wameanza masomo.

Halmashauri nyingine ambazo zimepata fedha za ujenzi wa sekondari mpya ni Manispaa ya Songea katika Kata ya Mshangano zimetolewa shilingi milioni 470 kujenga sekondari ya Luhira.

Kata nyingine ni ya Amanimakoro Halmashauri ya Mbinga,Kata ya Riwundi wilaya ya Nyasa,Kata ya Lituta Halmashauri ya Madaba na Kata ya Kizuka Halmashauri ya wilaya ya Songea.

Serikali imetoa jumla ya shilingi bilioni 7.7 kujenga sekondari mpya 11 katika Mkoa wa Ruvuma kupitia program ya  kuboresha Elimu ya sekondari nchini (SEQIUP).

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Februari 9,2023.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.