• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RUVUMA yang'aa kwenye ramani ya maendeleo;uwekezaji wa Trilioni 1.8 wageuza maisha ya wananchi

Imewekwa kuanzia tarehe: June 23rd, 2025

Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeiandika upya historia ya maendeleo mkoani Ruvuma kwa kuwekeza zaidi ya shilingi trilioni 1.18, hatua inayogeuza maisha ya wananchi na kuufanya mkoa huo kuwa mfano wa kuigwa kitaifa katika sekta mbalimbali za kijamii na kiuchumi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Mary Makondo, amesema hayo wakati wa hafla ya utambulisho wa mradi mkubwa wa ujenzi wa barabara ya lami ya kilomita 60 kutoka Likuyufusi (Manispaa ya Songea) hadi Mkayukayu (Halmashauri ya Wilaya ya Songea), ambapo serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 110 kutekeleza mradi huo kwa kipindi cha miezi 27.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, alibainisha kuwa maendeleo haya si ya bahati nasibu bali ni matokeo ya dhamira ya dhati ya Serikali ya Rais Samia kuweka ustawi wa mwananchi mbele.

Alisema Serikali imetumia shilingi bilioni 192.3 katika sekta ya elimu ambapo vyumba vya madarasa 1,717 vimejengwa, shule mpya 67 zimeanzishwa, mabweni 95, maabara 98, na nyumba za walimu 106 zimejengwa kwa viwango vya kisasa.

 Alisema serikali imewekeza bilioni 45.3 kwenye sekta ya afya kwa kujenga vituo vya afya 16, hospitali za wilaya 5, zahanati 47, na kuimarisha Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma.

 Aliongeza kuwa Vifaa tiba vya kisasa, magari ya wagonjwa 21, na magari maalum ya kusambaza chanjo vimeongeza upatikanaji wa huduma.

Makondo alisema Kwa kutumia shilingi bilioni 301.2, Serikali imejenga barabara ya lami Mbinga–Mbambabay (66 KM), barabara nyingine za lami zenye urefu wa 141.75 KM, na madaraja makubwa yenye urefu wa 231.5M.

Alisema  Miundombinu hii imeunganisha wilaya, kupunguza gharama za usafirishaji na kuongeza kipato cha wakulima waliokuwa hawana soko la uhakika.

Kwa uwekezaji wa shilingi bilioni 168.7, vijiji vyote 554 vya Mkoa wa Ruvuma sasa vinaunganishwa na gridi ya taifa. Hali hii imefungua fursa za biashara ndogo, viwanda vidogo na ujasiriamali wa wanawake na vijana.

 “Tunaangalia runinga na watoto wanasoma hadi saa nne usiku,” anasema Bi Frida Ligola wa Kijiji cha Lundo, Wilaya ya Nyasa.

Kulingana na Katibu Tawala huyo,Serikali imetumia bilioni 228.92 kuboresha huduma ya maji, ikiwa ni pamoja na mradi mkubwa wa maji wa bilioni 145 katika Manispaa ya Songea ambao unatarajiwa kumaliza tatizo la mgawo wa maji.

Kuhusu sekta ya usafiri,amesema Serikali imetumia shilingi bilioni 141 kuboresha usafiri kwa kukarabati Uwanja wa Ndege wa Songea, kujenga bandari za kisasa Ndumbi na Mbamba Bay, na vituo vya mabasi vya kisasa. .

Katika sekta ya kilimo, serikali imetumia bilioni 96.8 kujenga maghala 28, kusambaza tani 118,292 za mahindi na pembejeo.

Chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, maendeleo hayabahatishi tena; yanapangwa, yanatekelezwa, na yanaishi kwenye macho ya kila mwananchi wa Ruvuma.

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RUVUMA yang'aa kwenye ramani ya maendeleo;uwekezaji wa Trilioni 1.8 wageuza maisha ya wananchi

    June 23, 2025
  • KISIMA cha maji chawakomboa wananchi Luhangarasi Nyasa

    June 23, 2025
  • KITUO cha polisi cha kisasa chafunguliwa Namtumbo kwa gharama ya milioni 798

    June 22, 2025
  • JENISTA MHAGAMA akabidhi mashine na ng'ombe Peramiho

    June 22, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.