• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RUWASA Kuchimba visima kumi Tunduru

Imewekwa kuanzia tarehe: February 9th, 2025

Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Wilaya ya Tunduru, Mkoa wa Ruvuma, umeanza kutekeleza programu ya uchimbaji wa visima 900 nchini, ambapo kila jimbo linapata visima vitano. 

Katika Wilaya ya Tunduru, yenye majimbo mawili ya Uchaguzi—Tunduru Kusini na Kaskazini—jumla ya visima 10 vinachimbwa kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 600.

Afisa Maendeleo ya Jamii wa RUWASA Wilaya ya Tunduru, Leticia Mwageni, amesema mradi huo unalenga vijiji ambavyo havina miradi ya maji ya bomba ili kutatua changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi. 


Miongoni mwa vijiji vinavyonufaika ni kijiji cha Angalia, kata ya Mtina, ambacho kinapata kisima kinachojengwa kwa gharama ya shilingi milioni 60 kwa kutumia mafundi wa ndani.

Mwageni ameeleza kuwa RUWASA imenunua vifaa vyote vinavyohitajika ili kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati. 

Tayari ujenzi wa kituo cha kuchotea maji (kioski) umeanza, na matarajio ni kwamba ndani ya mwezi mmoja wananchi wataanza kupata maji safi na salama.


“Wilaya ya Tunduru ina majimbo mawili—Tunduru Kusini na Kaskazini—ambapo Jimbo la Tunduru Kusini limepata visima vitano kwa gharama ya shilingi milioni 300, huku Jimbo la Tunduru Kaskazini likipata visima vitano pia,” 

Kaimu Mtendaji wa Kijiji cha Angalia, Ramadhan Nyenje, ameishukuru serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kupeleka mradi huo wa maji katika kijiji hicho ambacho hakijawahi kuwa na maji ya bomba tangu Uhuru mwaka 1961. 

Amesema kijiji hicho chenye wakazi zaidi ya 6,332 kilikuwa kinategemea vyanzo vya asili kama mito na mabonde, ambavyo havitoshelezi mahitaji yao.

Ameongeza kuwa mradi huo utasaidia kupunguza muda wa kusubiri maji kwenye mabomba machache, na kwa kuwa ujenzi wake uko karibu na Shule ya Msingi ya kijiji hicho, wanafunzi watafaidika kwa kupata maji safi ya kunywa, kupikia na kusafisha mazingira yao.

Mkazi wa kijiji cha Angalia Zena Ismail, ameiomba RUWASA kuharakisha ujenzi wa mradi huo na kuweka mabomba kwenye makazi yao ili maji yaweze kufika majumbani, badala ya kutegemea vituo vya kuchotea maji. 


Amesema kwa sasa wanategemea vyanzo vya maji vya asili ambavyo siyo salama, lakini hawana mbadala, hivyo mradi huo utawapunguzia adha ya kutembea umbali mrefu kutafuta maji.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.