• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SEMENI mazuri aliyoyafanya Rais Samia Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: February 13th, 2023

VIONGOZI wa Chama cha Mapinduzi Mkoani Ruvuma wametakiwa kuyasema mazuri yote yanayofanywa na Rais, Wabunge na Madiwani ili wananchi waelewe kwa uwazi mambo hayo ambayo kimsingi yameainishwa kwenye ilani ya Ccm ya mwaka 2020/ 2025

Hayo yameelezwa  na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho kwenye Mkutano Mkuu wa Jimbo la Songea Mjini wa kupokea Utekelezaji wa Ilani ya CCM Katika Kipindi Cha Miaka mitano tangu 2018 - 2023 ya Uongozi wa Dkt.Damas Ndumbaro Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini na Waziri Wa Katiba na Sheria, Ulioifanya Songea Mjini.

Mwisho alisema kuwa yapo ambayo yamefanyika na yanaonekana kwenye sekta mbalimbali lakini viongozi wa Ccm kwenye maeneo yenu hamyatangazi, hali ambayo inapelekea kuzuka kwa masikitiko kwa wananchi

Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt Ndumbaro ameyaeleza mafanikio aliyoyapata kwa miaka mitano toka 2018-2023 na ameyaandika kwenye kitabu chenye kurasa 140, myasome na myaeleze waziwazi ili wanachama na wananchi wayaelewe namna Mbunge anavyohangaika kuwaletea maendeleo

“Nakupongeza sana Mbunge Dkt Ndumbaro kwa kazi kubwa unayoifanya katika Jimbo lako na Nchi kwa ujumla, sie kama chama ndio tulikukabidhi Ilani ili uitekeleza hakika umefanya makubwa kwa muda mfupi, hongera sana na tutaendelea kuyasema haya kila mara ili kukirahisishia chama katika uchaguzi wa Serikali za mitaa na vijiji mwaka 2024 na uchaguzi mkuuu mwaka 2020” alisema Mwisho

Akisoma ilani hiyo ya miaka mitano Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt Damas Ndumbaro ambaye pia ni Waziri wa Sheria na Katiba alisema kuwa mambo mengi yametekelezwa katika sekta zote na kuwafanya wananchi waendelee kufurahia uwepo wa Viongozi wanaotokana na Ccm

Dkt Ndumbaro alisema katika kipindi cha mwaka 2018 hadi 2023 Serikali imetekeleza na kuendeleza miradi mbalimbali ikiwemo na ujenzi wa vyumba vya madarasa fedha za UVIKO 19, ujenzi wa vituo vya afya vipya vitano 5 na Hospitali ya Wilaya 1 pamoja na Hosptali ya Rufaa ya Mkoa 1 iliyopo Mwengemshindo,

“Kujengwa Chuo kikuu kipya cha Uhasibu Arusha, Masoko mawili ya kisasa (Manzese), ujenzi wa uwanja wa ndege, daraja ya Matarawe- Mjiwema, Mikopo kwa vikundi bil. 1 kwa mwaka, Barabara kutoka Sanga one hadi Tanroad, kujenga barabara ya kiwango cha Lami km 13 katika kata ya Mfaranyaki, Misufini, na Majengo na miradi mingineyo kutawafanya wananchi kupiga hatua ya kimaendeleo” alisema Dkt Ndumbaro.

Alisema pamoja na ukarabati wa miundombinu chakavu ya madarasa, barabara za mitaa, maji kwa baadhi ya kata, uhitaji wa vituo vya afya katika kata ya Bombambili, Ruhuwiko, na Lizaboni, uhitaji wa shule za Sekondari mpya kwa kata ambazo hazina Sekondari za kata kama Seedfarm, Ruhuwiko na Ndilima Litembo.

Naye Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano amesema Manispaa imetenga bajeti ya shilingi Mil. 20 kupeleka kila kata ambazo zitasaidia kutatua changamoto mbalimbali za kata husika ikiwemo ukarabati wa miundombinu ya madarasa chakavu.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Dkt, Frederick Sagamiko alisema changamoto ya barabara za mitaa haita kuwepo kwa sasa kwani Manispaa imeandaa utaratibu kupitia TARURA wa kutatua chanagamoto hizo ambapo ameagiza kata zote 21 kuleta taarifa zenye ufafanuzi maalum wa mahitaji ya miundombinu korofi ambayo inahitaji kutekelezwa ikiwemo na barabara za mitaa, vivuko vyote, madaraja, na mifereji ili TARURA waweze kutekeleza .

Mwenyekiti wa CCM Wilaya Songea Mjini Mwinyi Msolomi amewataka Viongozi mbalimbali kuacha Mipasuko ambayo itapelekea kuzorotesha shughuli za kimaendeleo.

Msolomi alisema lengo kuu la Serikali katika kuaajiri wataalamu ni kwa ajili ya kusimamia na kuratibu shughuli shughuli zote za Serikali pamoja na kusogeza huduma kwa wananchi,

Kwa upande wake Katibu wa CCM Wilaya ya Songea Mjini James Mgego alisema kuwa Wananchi wa Songea wana kila sababu ya kumshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya ikiwemo kutoa fedha nyingi ambazo zimekwenda kutekeleza miradi mbalimbali

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.