• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI ilivyodhamiria kujenga chuo kikuu cha Uhasibu Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: May 6th, 2025

Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa shilingi bilioni 18.5 kwa ajili ya ujenzi wa kampasi ya Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) katika Manispaa ya Songea, Mkoa wa Ruvuma.

Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja wa IAA Kampasi ya Songea, Dkt. Bakari Mashaka alisema kuwa ujenzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya Rais Samia kuhakikisha kila mkoa unakuwa na chuo kikuu ili kuboresha elimu ya juu nchini.

Kwa mujibu wa Dkt. Mashaka, chuo hicho kipya kitakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 10,000 na kitaanza kujengwa mara moja kwa kutumia mfumo wa ‘force account’. Alisema kwa sasa IAA Kampasi ya Songea inatoa kozi mbalimbali zikiwemo za diploma na shahada katika nyanja za biashara, uhasibu, fedha, benki, TEHAMA na uongozi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha, Dkt. Mwaitete Cairo, alieleza kuwa Manispaa ya Songea imetoa eneo lenye ukubwa wa hekari 71 katika Kata ya Tanga kwa ajili ya ujenzi huo. Alibainisha kuwa mradi huo utatoa ajira kwa wakazi wa Songea pamoja na kuchochea shughuli za kiuchumi kutokana na uwepo wake karibu na miundombinu kama stendi kuu ya mabasi, machinjio ya kisasa na hospitali ya rufaa.

Afisa Uhusiano wa IAA Kampasi ya Songea, Nuru Meshack, aliwahamasisha vijana kuchangamkia fursa za elimu akibainisha kuwa hata wanafunzi waliopata daraja la nne wanaweza kujiunga na masomo ya diploma, kinyume na imani ya baadhi ya wazazi.

Meya wa Manispaa ya Songea, Michael Mbano, alilipongeza chuo hicho kwa hatua hiyo na kusema kuwa limejibu kilio cha muda mrefu cha wananchi kutaka taasisi za elimu ya juu mkoani humo.

Wakati huo huo, IAA imejipanga kuanzisha madarasa ya mtandaoni ili kutoa elimu kwa wanafunzi walioko katika kampasi zake za Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Babati, Songea na hata nje ya nchi ikiwemo Sudan Kusini na Comoro, hatua itakayowezesha mafunzo kutolewa kwa wakati mmoja kimataifa

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.