• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI ilivyodhamiria kumaliza kero ya maji Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: March 16th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed amesema Halmashauri zote nane zimefikia kiwango cha kuridhisha cha upatikanaji wa maji ambapo tayari miradi 23 ya maji iliyogharimu shilingi bilioni 25.9 imekamilika.

Kanali Abbas amesema hayo wakati anazungumza na wanahabari ofisini kwake mjini Songea,kuelekea katika maadhimisho ya wiki ya maji ngazi ya Mkoa wa Ruvuma ambayo yanaanza Machi 16 hadi 22 mwaka huu.

Amebainisha kuwa upatikanaji wa maji vijijini katika Halmashauri ya wilaya ya Songea umefikia asilimia 78.1,Madaba asilimia 79.4,Tunduru asilimia 70.2,Halmashauri ya Mbinga asilimia 71,Mbinga Mji asilimia 76,Namtumbo asilimia 71 na Nyasa asilimia 60.1.

Hata hivyo amesema licha ya miradi hiyo iliyokamilika,kuna miradi ya maji 30 inayoendelea kutekelezwa yenye thamani ya shilingi bilioni 58.5 na kwamba miradi hiyo ikikamilika itakuwa na uwezo wa kuhudumia wananchi 264,747 na kuongeza asilimia ya upatikanaji wa huduma ya maji toka asilimia 70.9 hadi 87.

“Ipo miradi 22 ya kipaumbele inayotekelezwa kwa thamani ya shilingi bilioni 8.6,pia serikali imetenga shilingi bilioni 18.9 za  kutekeleza miradi 38 ambayo itahudumia vijiji 66’’,alisema Kanali Abbas.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,Mkoa pia unatekeleza program ya visima 40 kwa wastani wa visima vitano kwa kila Jimbo ambapo tayari visima virefu 30   vimechimbwa katika majimbo ya Nyasa,Songea,Tunduru na Namtumbo.

Ameongeza kuwa baada ya kukamilika kwa mradi wa maji wa miji 28 unaotekelezwa katika Manispaa ya Songea kwa gharama ya Zaidi ya shilingi bilioni 145,upatikanaji wa maji katika Mkoa wa Ruvuma utafikia katika kiwango cha wananchi wote kupata huduma ya maji safi na salama.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma Komredi Odo Mwisho akizungumza kwenye mkutano huo na wanahabari  amemshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuleta fedha nyingi za kutekeleza miradi ya maji katika Mkoa wa Ruvuma.

Amesema kabla ya uongozi wa serikali ya Awamu ya Sita upatikanaji wa maji katika Mkoa wa Ruvuma ulikuwa ni  chini ya asilimia 50 kwa uongozi  wa awamu ya kwanza hadi ya Tano ambapo katika Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan  upatikanaji wa maji umepanda kwa kiwango kikubwa hadi kufikia Zaidi ya asilimia 78.

Amesema kuwa hali hiyo inaonesha kuwa Rais Samia amedhamiria kwa vitendo kumtua mama ndoo  kichwani na kumaliza kabisa kero ya upatikanaji wa  maji na salama kwa wananchi 

Kaulimbiu ya maji wiki ya maji mwaka huu ni Uhifadhi uoto wa asili kwa uhakika wa maji

Pichani ni Mwenyekiti wa CCM Ruvuma Komred Oddo Mwisho akizungumza na wanahabari kuelekea maadhimisho ya wiki ya maji  Ruvuma


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MSIKIMBILIE hasara,serikali inakuja na bei ya neema kwa mahindi Julai

    May 31, 2025
  • WAKULIMA Namtumbo wachuma neema ya ufuta kwa teknlojia mpya ya mnada wa kidigitali

    May 31, 2025
  • RUSHWA yazidi kuporomoka na kukosa nafasi Ruvuma

    May 31, 2025
  • SERIKALI yatoa fidia ya bilioni 2.5 kupisha mradi wa umeme wa Grid Songea-Tunduru

    May 31, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.