• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI inavyoendelea kuimarisha miundombinu ya barabara na madaraja Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: May 23rd, 2025

Serikali kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS) inaendelea na juhudi za kuboresha miundombinu ya barabara na madaraja mkoani Ruvuma.

Lengo kuu ni kurahisisha usafiri na usafirishaji wa bidhaa, hivyo kuchochea uchumi na kupunguza umaskini.

TANROADS Mkoa wa Ruvuma inasimamia mtandao wa barabara wa kilomita 2,166.62, zikiwemo barabara kuu na barabara za mkoa.

BAJETI NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

Meneja wa TANROADS Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Salehe Juma Mkwama anasema Katika kutekeleza majukumu yake, TANROADS inasimamia miradi mikubwa ya maendeleo, miradi midogo ya maendeleo, pamoja na matengenezo ya barabara na madaraja.

Miradi hii inatekelezwa kwa bajeti inayosimamiwa kupitia Makao Makuu ya TANROADS kwa kushirikiana na serikali na wadau wa maendeleo.

MIRADI MIKUBWA YA MAENDELEO

 UJENZI WA BARABARA YA MBINGA – MBAMBA BAY

Barabara hii ya kilomita 66 ilijengwa na kampuni ya China Henan International Cooperation Group Co. Ltd (CHICO) kwa gharama ya Tsh. 129.36 bilioni. Mradi huu ulizinduliwa tarehe 24 Septemba 2024 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan.

 UJENZI WA DARAJA LA RUHUHU

Daraja  la Ruhuhu lililopo katika Mto Ruhuhu unaomwaga maji yake ziwa Nyasa\, lina urefu wa mita 98.01 linaunganisha Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma na Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe. Ujenzi  wa daraja hilo ulikamilika tarehe 15 Oktoba 2021 kwa gharama ya Tsh. 8.976 bilioni.

UKARABATI WA UWANJA WA NDEGE SONGEA

Ukarabati wa uwanja huu ulianza Aprili 2019 na kukamilika Machi 2023 kwa gharama ya Tsh. 37.09 bilioni. Mradi huu ulikuwa kwenye kipindi cha uangalizi hadi Septemba 2024.

UJENZI WA BARABARA YA KITAI - LITUHI - NDUMBI

Mradi huu wa kilomita 95.3 unatekelezwa kwa awamu tatu kwa kiwango cha lami:

• Kitai – Amani Makoro (Km 5): Ulianza Juni 2019 na kukamilika Agosti 2020 kwa Tsh. 6.957 bilioni.

• Amani Makoro – Ruanda (Km 35): Ujenzi ulianza Juni 2022  kwa Tsh. 60.481 bilioni.

• Ruanda – Lituhi – Ndumbi (Km 50): Ujenzi unaendelea kwa Tsh. 95.76 bilioni na unatarajiwa kukamilika Juni 2026.

 UJENZI WA BARABARA YA LIKUYUFUSI – MKENDA

Barabara hii ya kilomita 124 ipo kwenye hatua za mwisho za kusainiwa kwa mkataba wa ujenzi. Fidia ya Tsh. 5.19 bilioni imeshatathminiwa na kusubiri malipo kutoka Wizara ya Fedha.

 UJENZI WA BARABARA YA LUMECHA–LONDO-MALINYI – LUPIRO

Mradi wa ujenzi wa barabara hii ya kilomita 512 inaunganisha
mikoa ya Ruvuma na Morogoro.

 Serikali imesaini mkataba na kampuni ya China Civil Engineering ConstructionCorporation Ltd (CCECC) kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huu 

kwa sasa utatekelezwa kwa Mfumo wa Sanifu na jenga ('Design and Build')  ambao ni ujenzi wa barabara ya Lumecha - Londo - Malinyi - Lupiro 

UJENZI WA BARABARA YA SONGEA – LUTUKIRA NA MCHEPUKO WA SONGEA

Mradi huu wa kilomita 116 unafadhiliwa na Benki ya Dunia. Ujenzi unatarajiwa kuanza wakati wowote baada ya kukamilika kwa mchakato wa zabuni.

MIRADI YA MADARAJA

DARAJA LA MITOMONI

Daraja lenye urefu wa mita 47.7 linaunganisha Wilaya za Nyasa na Songea Vijijini.

Mradi huu utatekelezwa kwa miezi 15 kwa gharama ya Tsh. 9.29 bilioni kwa ufadhili wa Serikali na Benki ya Dunia.

DARAJA LA MKILI

Daraja hili linafanana na la Mitomoni na linajengwa kwa Tsh. 3.19 bilioni kwa muda wa miezi 15.

DARAJA LA MKENDA

Daraja hili linaunganisha Tanzania na Msumbiji kupitia Mto Ruvuma. Zabuni yake ilitangazwa lakini ilihitajika kutangazwa upya baada ya mzabuni mmoja tu kujitokeza.

USANIFU WA BARABARA NA MADARAJA

Mbali na miradi inayoendelea, TANROADS inaendelea na usanifu wa barabara na madaraja muhimu kama:

• Barabara ya Mbamba Bay – Lituhi (Km 112.4)

• Barabara ya Mtwarapachani – Nalasi – Tunduru (Km 300)

• Barabara ya Madaba – Mundindi – Liganga – Mkiu (Km 46)

MATENGENEZO YA BARABARA NA HIFADHI YA BARABARA

Katika kuhakikisha barabara zinapitika muda wote, TANROADS mkoa wa Ruvuma imetenga Tsh. 17.9 bilioni kwa ajili ya matengenezo ya barabara za muda maalumu na sehemu korofi.

Aidha, jitihada za kuhifadhi hifadhi ya barabara zinaendelea kwa kuweka vigingi na kutoa notisi kwa wavamizi.

Juhudi za serikali kupitia TANROADS mkoa wa Ruvuma zinaendelea kuleta maendeleo kwa kuboresha miundombinu ya barabara na madaraja.

Haya yote yanalenga kuinua uchumi wa wananchi kwa kurahisisha usafiri, kuunganisha mikoa na kuimarisha sekta ya uchukuzi nchini.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Miaka minne ya mageuzi makubwa ya elimu Ruvuma,shule zaota kama uyoga kila kona

    May 23, 2025
  • SERIKALI inavyoendelea kuimarisha miundombinu ya barabara na madaraja Ruvuma

    May 23, 2025
  • CHANZO cha Mto Ruvuma na maporomoko ya Nakatuta urembo wa asili unaovutia wengi

    May 23, 2025
  • DED Madaba apongeza huduma za afya za hospitali ya Halmashauri

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.