• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI kuweka mfumo wa wazi wa uuzaji kahawa

Imewekwa kuanzia tarehe: September 22nd, 2024


Serikali imewahakikishia wakulima na wamiliki wa viwanda vya kukoboa Kahawa nchini kuwa itatengeneza utararibu wa kuuza kahawa ili kuwa na mfumo wa uwazi wenye bei itakayomnufaisha mkulima kwa kuchagua bei anayoitaka.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (Mb) alipofanya ziara ya ukaguzi katika Kiwanda cha Kupokea na Kukoboa Kahawa aina ya “Arabica” (Mbinga Coffee Curing Company) kilichopo Mbinga, mkoani Ruvuma .

“Lazima tuongeze tija kwa wazalishaji wa kahawa. Hivyo, niwahakikishie kuwa Serikali itaendelea kutoa miche ya ruzuku ya kahawa ambayo inazalishwa na TACRI, tutaanzisha mfumo wa ruzuku za pembejeo, tutachimba visima kusaidia wakulima na kujenga ghala la kuhifadhi kahawa zao,” amesema Waziri Bashe.

Kuhusu wafanyabiashara wanyonyaji kwa wakulima (kangomba), Serikali itachukua hatua dhidi ya unyonyaji huo kwa wakulima. Waziri Bashe amesema kuwa ushirika imara siyo unaonyonya wakulima; na hivyo wakulima kupitia vyama vya ushirika na waliopo katika vikundi mbalimbali washiriki katika mfumo wa Soko la Bidhaa Tanzania (TMX) linalosimamia mnada wa kijiditali ili kuwaongezea uhakika wa masoko, uhuru wa kuamua bei, uhakika wa malipo yao pamoja na kuchochea ushindani.

Aidha, Waziri Bashe amehamasisha wazalishaji wa Kahawa nchini kama vile aina ya Mbinga Café kuwa na kampeni bunifu za kunadi upekee / utofauti wa kubidhaisha Kahawa zao ili kuvutia biashara. Ametolea mifano kama vile hadithi au simulizi kuhusu Kahawa ya kampuni fulani, au viungo / ladha / virutubisho vilivyomo kwenye Kahawa husika.

Mbinga Coffee Curing Company inamilikiwa na Vyama vya Ushirika 28 vinavyolima Kahawa nchini kwa asilimia 56.54, huku Serikali ikimiliki asilimia 43.46 ambapo kiwanda chake kilianza ukoboaji wa Kahawa mwaka 1989. Kiwanda kina uwezo wa kukoboa tani 10 kwa saa moja, na uwezo wa kukoboa tani 30,000 kwa mwaka.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • KIONGOZI Mwenge wa uhuru ashiriki upandaji miti Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru waweka jiwe la msingi shule ya amali Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru wazindua jengo la EMD Peramiho

    May 10, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.