• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI wilayani Mbinga yakazia wito wa RC Ibuge

Imewekwa kuanzia tarehe: October 25th, 2021

Wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla wamekumbushwa kulipa kodi kwa wakati kwasababu kodi hiyo hurudi kwao kupitia miundombinu na miradi mbalimbali ya maendeleo.

Wito huo ambao awali ulitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge ambapo sasa umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mbinga,Aziza Mangosongo wakati akizungumza na timu ya maofisa kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Makao Makuu Dar es Salaam walipowasili wilayani humo kwa ajili ya kufanya kampeni ya elimu kwa mlipakodi mlango kwa mlango.

Aziza amesema kuwa, kodi hulipwa na watu wote wakiwemo watumishi wa serikali na wa sekta binafsi, wakulima, wafugaji, wavuvi pamoja na wafanyabishara, tofauti ni kwamba, kodi inayolipwa na watumishi hukatwa moja kwa moja kupitia mishahara yao.

“Napenda kuchukua fursa hii kuwahamasisha na kuwakumbusha wafanyabiashara na wananchi wote kulipa kodi kwa wakati ili kuinua uchumi wa nchi yetu na tuondoe ile kasumba ya kusema kwamba watumishi wa serikali hawalipi kodi, watumishi tunakatwa kodi moja kwa moja kupitia mishahara yetu,” amesema Mangosongo.

Aidha, Aziza amewataka wananchi kuwafichua watu wanaokwepa kulipa kodi kwa kutoa taarifa sahihi za wahusika hao katika maeneo mbalimbali ili washughulikiwe.

“Pia, nawaomba tusisite kuwataja watu wote wanaokwepa kulipa kodi na tujitahidi kutoa taarifa sahihi za wakwepa kodi katika maeneo yetu kwa maana kodi ni afya na ni uhai wetu,” amesema Aziza.

Naye, Meneja wa Huduma kwa Mlipakodi kutoka TRA Makao Makuu Honester Ndunguru amesema kuwa TRA imejipanga kuhakikisha inawafikia idadi kubwa ya wafanyabiashara nchini kwa ajili ya kuwaelimisha kuhusu haki na wajibu wao katika suala zima la ulipaji kodi.

“Sisi kama TRA, tumejipanga kufika maeneo mbalimbali kuhakikisha tunawaelimisha walipakodi wetu kujua haki na wajibu wao na leo tumekuja hapa Mbinga kwa lengo hilohilo la kuhakikisha tunawafikishia elimu ya kodi wafanyabiashara wa wilaya hii,” amesema Ndunguru.

Timu ya maofisa wanaofanya kampeni ya elimu kwa mlipakodi mkoani Ruvuma wako wilayani Mbinga wakiendelea kutoa elimu ya kodi na baada ya wilaya hiyo wataelekea Wilaya za Nyasa, Namtumbo na Tunduru.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.