• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI wilayani Songea yawaagiza wafanyabiashara waliogoma kurudisha huduma ndani ya saa 24

Imewekwa kuanzia tarehe: February 22nd, 2021


 SERIKALI wilayani Songea mkoani Ruvuma imewaagiza wafanyabiashara na wasafirishaji abiria waliogoma kurudisha huduma zao ndani ya saa 24 kuanzia saa tisa alasiri Februari 22,2021.

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Songea Cosmas Nshenye akizungumza na wanahabari ofisini kwake mjini Songea, amesema kufuatia mgomo unaoendelea amemwagiza Afisa LATRA kufuta mara moja route ya mabasi yote yanayotoa huduma ya usafirishaji kuanzia Songea mjini hadi Mbinga mjini.

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya ametoa rai kwa wafanyabiashara wote wenye nia ya kutoa huduma za usafirishaji abiria kutoka Songea mjini hadi Mbinga waombe mara moja kufanya shughuli za usafirishaji katika route hiyo.

Amesema serikali itaendelea kufuatilia mwenendo wa route nyingine za usafirishaji ili kuona ufanisi wake katika kuhudumia wananchi.

“Tuna taarifa kupitia vikao vya wafanyabiashara vilivyofanyika hivi karibuni kuwepo kwa matamshi ya lugha za matusi,uchochezi na uvunjifu wa amani na kuhujumu mipango ya serikali katika kutoa huduma kwa wananchi,hivyo naliagiza Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi mara moja na kuchukua hatua stahiki za kisheria kwa wahusika wote watakaobainika kuhusika na vitendo  hivyo’’,alisisitiza Mkuu wa Wilaya.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya ameliagiza Jeshi la polisi  na LATRA kuweka mpango mbadala wa haraka wa utatuzi wa suala la usafiri katika kurudisha huduma za usafiri ili kuondoa kero hiyo kwa wananchi.

Mkuu wa Wilaya pia amemwagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea na LATRA kuwachukulia hatua za kisheria kwa mujibu wa Sheria za Leseni ikiwemo kuwanyang’anya leseni za biashara wahusika wote watakaokaidi maelekezo ya kurudi kazini na kufungua biashara zao ndani ya saa 24 kuanzia saa tisa alasiri Februari 22,2021.

Amesisitiza kuwa serikali itaendelea kusimamia matumizi ya stendi ya Mfaranyaki kama ilivyoamiriwa kupitia vikao vya kisheria vya Baraza la madiwani  la Manispaa ya Songea kwa ajili ya matumizi ya usafiri wa daladala na sio vinginevyo.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Februari 22,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.