• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yaendeleza ujenzi barabara ya Amanimakoro-Ruanda

Imewekwa kuanzia tarehe: March 7th, 2025

Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Ruvuma umeanza ujenzi wa awamu ya pili wa barabara ya Amanimakolo-Ruanda hadi Bandari ya Ndumbi yenye urefu wa kilometa 95 kwa kiwango cha lami. 

Meneja wa TANROADS Mkoa wa Ruvuma,Mhandisi Saleh Juma, amesema ujenzi huo utafanyika kwa awamu tatu, ambapo awamu ya kwanza iliyohusisha kilometa tano kutoka Kitai hadi Amanimakolo tayari imekamilika na barabara hiyo imeanza kutumika.

Kwa sasa, ujenzi wa awamu ya pili unaendelea kutoka Amanimakolo hadi kijiji cha Ruanda, umbali wa kilometa 35. Meneja huyo amebainisha kuwa kazi imeanza kwa kuweka tabaka la lami kwenye kipande cha kilometa mbili kati ya 35.

 Aidha, ujenzi huu ni sehemu ya mafanikio ya miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, ambapo awamu ya tatu itahusisha kipande cha Ruanda hadi Bandari ya Ndumbi wilayani Nyasa.

Saleh ameongeza kuwa ujenzi wa Bandari ya Ndumbi ulikamilika miaka miwili iliyopita na kinachosubiriwa ni ukamilishaji wa barabara ili bandari hiyo ianze kutumika kusafirisha bidhaa kutoka Ruvuma kwenda mikoa mingine na nchi jirani ya Malawi.

 Alisisitiza kuwa TANROADS inaendelea kutekeleza mradi huu bila vikwazo, huku Serikali ikiendelea kutoa fedha kwa ajili ya kukamilisha kazi hiyo ili kuondoa kero ya vumbi linalosababishwa na magari yanayosafirisha makaa ya mawe.

Kwa upande wake, Mhandisi wa TANROADS Ruvuma, Anselem Chambila, amesema kati ya kilometa 35 zilizopo kwenye mpango wa awamu ya pili, kilometa tano tayari zimeanza kujengwa na mbili ziko katika hatua za mwisho kukamilika. Ameeleza kuwa mradi huu unatekelezwa vizuri na wanachosubiri ni fedha za kukamilisha kipande kilichobaki ili wananchi waweze kunufaika na barabara hiyo.

Naye Meneja Mradi wa Kampuni ya China Railway Seventh Group (CRSG), GE Guanghua, amesema hadi sasa utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 40. Wakati huo huo, baadhi ya wananchi wa kijiji cha Amanimakolo wameipongeza Serikali kwa kuendelea na ujenzi wa barabara hiyo, huku wakiitaka TANROADS kumsimamia kwa karibu mkandarasi ili kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati na kuondoa adha ya usafiri.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.