• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI kumega hekta 33,000 kuwapatia wananchi Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: December 31st, 2022

Serikali itamega jumla ya hekta 33,132.24 katika mkoa wa Ruvuma kutoka maeneo ya hifadhi na shamba la NAFCO na kubakizwa kwa wananchi kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

Aidha, imeelekeza wananchi wote waliovamia Hifadhi ya Msitu wa Lihanje uliopo halmashauri ya wilayani Songea kusitisha shughuli zozote za kibinadamu katika maeneo ya mlimani na bondeni mwaka huu,

Hayo yameelezwa tarehe 30 Desemba 2022 na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula katika kikao cha Kamati ya Mawaziri Nane wa Wizara za Kisekta na uongozi wa mkoa wa Ruvuma wakati Kamati hiyo ilipofanya ziara kwa ajili ya kutoa mrejesho wa Maamuazi ya Baraza la Mawaziri kuhusiana na Utatuzi wa Migogoro ya Matumizi ya Ardhi katika vijiji 975.

Dkt Mabula ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mawaziri Nane wa Wizara za Kisekta alisema, mkoa wa Ruvuma unahusisha vijiji/mitaa 38 yenye migogoro ya matumizi ya ardhi ambapo maamuzi ya Kamati ni kumega sehemu ya maeneo  ya hifadhi kuwaachia wananchi  sambamba  na kusitishwa shughuli za kibindamu kwenye hifadhi .

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, wakati wa zoezi la tathmini kuhusu migogoro ya matumizi ya ardhi kwenye mkoa wa Ruvuma timu ya wataalamu ilivifikia vijiji/mitaa 38 katika wilaya za Mbinga, Nyasa, Tunduru, Namtumbo na Songea ambapo zoezi la uwandani lilihusisha na kufanya vikao na uongozi wa serikali za vijiji husika na kisha kutembelea maeneo yenye migogoro.

‘’Pamoja na maamuzi haya ya serikali ya kumega maeneo kwa ajili ya vijiji mkoa unalo jukumu la kusimamia utekelezaji wa maamuzi hayo kwa kusimamia utekelezaji huo kwa kushirikiana na taasisi na mamlaka zote zilizopo ndani ya mkoa na ni muhimu maeneo haya yaliyomegwa kuandaliwa mpango wa matumizi ya ardhi ili kuepuka matumizi holela ’’ alisema Dkt Mabula

Akigeukia umauzi wa serikali kusitisha shughuli za kibinadamu kwa wananchi waliovamia hifadhi ya msitu wa Lihanje, Dkt Mabula ameelekeza mkoa kwa kushirikiana na timu atakayoiunda kufanya tahmini ya kina ya mahitaji halisi ya ardhi kulingana na idadi ya watu waliopo katika vijiji hivyo na kuahidi timu yake ya mawaziri wa wizara za kisekta kurejea tena mapema januari 2023 kwa ajili ya kupokea taarifa na kutoa maamuzi.

‘’wananchi wote waliovamia hifadhi yam situ wa Lihanje kwa kuendesha shughuli za kilimo kwa maeneo ya mlimani na bondeni wanaelekezwa kusitisha shughuli zozote za kibinadamu katika maeneo hayo kwa mwaka huu’’ alisema Dkt Mabula.

Msitu wa Lihanje unasimamiwa na Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) na ni vyanzo muhimu vya maji vyenye mradi wa maji mtiririko Luyelela na Kilagano ambapo wananchi wamevamia takriban asilimia 60 ya msitu na kuendesha shughuli za kilimo,

Aliushukuru mkoa wa Ruvuma kwa kuweza kuratibu vyema zoezi la tahmini alilolieleza kuwa limewezesha kazi hiyo kufanyika kwa amani na utulivu huku akitambua mkoa huo unazo changamoto nyingi zinazosababishwa na muingiliano wa matumizi ya ardhi.

Kwa upande wake Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt Pindi Chana amewataka wananchi kukemea wale wanaoharibu vyanzo vya maji na kuzitaka mamlaka zote kuanzia ngazi ya vijiji kuhakikisha zinadhibiti uvamizi wowote unaofanyika katika hifadhi za misitu na mapori ya akiba.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Ruvuma Comredi Odo Mwisho amesema chama chake kinaungana na serikali kuhakikisha inalinda maeneo yote yaliyotamkwa kuwa ni hifadhi ya asili ili kuepuka uharibifu wa mazingira n auto wa asili.

Timu ya Mawaziri Nane wa Wizara za Kisekta imehitimisha ziara yake katika mkoa wa Ruvuma na januari nne , 2023 inatarajiwa kuendelea na ziara yake katika mkoa wa Mara.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.