• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa bilioni 12.7 Ruvuma kutekeleza miradi ya Elimu,Afya na uchumi

Imewekwa kuanzia tarehe: October 20th, 2021

MKOA wa Ruvuma umepokea shilingi bilioni 12.7 sawa na asilimia 2.4 ya shilingi bilioni 635.68 ambazo zimeidhinishwa na TAMISEMI kwa ajili ya uboreshaji wa sekta ya Afya,Elimu na Uwezeshaji wananchi kiuchumi.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge katika kikao kazi cha maandalizi ya utekelezaji wa mpango wa Maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19 ,kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea 

“Matumizi ya fedha hizi yameelekezwa kwenye maeneo ya vipaumbele yanayogusa wananchi moja kwa moja ili kuwaondolea kero katika na kupata huduma za afya,elimu na uwezeshaji wananchi kiuchumi na kuwakinga dhidi ya UVIKO 19”’alisisitza RC Ibuge 

Akifafanua kuhusu fedha hizo Brigedia Jenerali Ibuge amesema sekta ya elimu imetengewa shilingi bilioni 10.32 kati ya fedha hizo elimu msingi imetengewa bilioni 1.36 kwa ajili ujenzi wa vyumba 52 vya madarasa na elimu sekondari imetengewa bilioni 8.96 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 448 vya  madarasa kwa ajili ya kujiandaa kupokea wanafunzi wa wa kidato cha kwanza Januari 2022.

Kwa upande wa sekta ya afya Brigedia Jenerali Ibuge amesema jumla ya shilingi bilioni 2.38 zimetengwa kwa ajili ya kuanzisha mfuko wa huduma za dharura ,kujenga jengo la wagonjwa mahututi na kununua mitambo miwili ya huduma za mionzi.

Mkuu wa Mkoa ameziagiza Halmashauri zote kusimamia ujenzi wa madarasa ya sekondari na kwamba ifikapo Desemba 30,2021 pasiwepo na upungufu tena wa vyumba vya madarasa na kusisitiza kuwa Halmashauri ambayo itakuwa na upungufu itumie vyanzo vya mapato ya ndani kujenga madarasa Hayo .

RC Ibuge amewaagiza watendaji kwenye Halmashauri zote kuhakikisha kuwa wakati wa utekelezaji wa miradi hiyo kuwashirikisha wananchi tangu hatua za awali za utambulisho wa miradi.

katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amempongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za kupambana na UVIKO 19,zilizowezesha nchi kupata mkopo wenye masharti nafuu wa shilingi trilioni 1.3 kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa IMF kwa ajili ya kampeni Maendeleo ya uchumi na mapambano ya UVIKO 19.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma 

Oktoba 20,2021



Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.