• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa bilioni 2.5 kwa TANROADS Ruvuma kurejesha miundombinu

Imewekwa kuanzia tarehe: May 7th, 2024

WAKALA wa barabara (TANROADS) Mkoa wa Ruvuma,umepokea Sh.bilioni 2.5 kati ya Sh.bilioni 6 ilizoomba ili kurejesha miundombinu ya barabara zilizoharibiwa na mvua za masika katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo.


Hayo yamesemwa  na Meneja wa TANROADS Mkoa wa Ruvuma  Mhandisi Saleh Juma,baada ya kukagua kazi ya urejeshaji wa miundombinu ya daraja la Mto maarufu la Namiungo wilayani Tunduru.
Saleh,amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan,kwa kuidhinisha fedha hizo ambazo zitatumika kwa ajili ya matengenezo ya barabara kwenye maeneo yenye changamoto ili kutoa fursa kwa shughuli za usafiri na usafirishaji kuendelea kama kawaida.


Amesema,licha ya mvua za masika kunyesha kwa wingi  katika Mkoa Ruvuma,barabara zote zilizo chini ya TANROADS zinapitika na hakuna shughuli za kijamii zilizosimama kutokana na ubovu wa barabara.

Mwezi Machi mwaka huu daraja la Namiungo lilipata athari kubwa baada ya maji ya mvua kupita juu ya daraja na kuharibu miundombinu,hali iliyosababisha magari kupita upande mmoja.
Meneja huyo wa TANROADS Mkoa wa Ruvuma amesema,kazi ya kurejesha miundombinu ya daraja hilo imechelewa kukamilika kutokana na changamoto ya mvua, ambapo magari ya mkandarasi yameshindwa kufika maeneo yanakopatikana mawe na vifusi.


Hata hivyo,amemtaka mkandarasi kuhakikisha anakamilisha kazi mwishoni mwa mwezi huu ili barabara hiyo irudi kwenye hali yake na wananchi waendelee kuitumia katika shughuli zao za uzalishaji mali.

Mhandisi wa kampuni ya Ovans Constructions Ltd iliyopewa kazi ya matengenezo ya daraja la Namiungo Azimio Mwapongo amesema,amehaidi kufanya kazi usiku na mchana ili waweze kukamilisha kazi mwisho wa mwezi huu.




Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.