• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa bilioni 3.6 kutekeleza miradi miwili Madaba

Imewekwa kuanzia tarehe: March 9th, 2021

SERIKALI ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt.John Magufuli imetoa shilingi bilioni 3.6 kutekeleza miradi miwili katika Halmashauri ya Madaba wilayani Songea mkoani Ruvuma.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Shafi Kassim Mpenda akizungumza katika mahojiano maalum ofisini kwake mjini Madaba amesema katika mradi wa kwanza serikali imetoa shilingi bilioni tatu kwa ajili ya kutekeleza mradi wa jengo la Halmashauri.

Mpenda amesema hadi sasa jengo hilo limekamilika kwa asilimia 100 ambapo jumla ya shilingi bilioni 2.914 zimetumika na kwamba mradi  huo umekamilika na jengo limeanza kutumika hivyo kutatua changamoto ya uhaba wa ofisi uliokuwa unawakabili watumishi wa Halmashauri hiyo na wananchi.

“Kwa ujumla wake katika kutekeleza mradi huu wa jengo la utawala,tulipokea shilingi bilioni tatu,mradi ulianza mwaka 2017 na umekamilika  kupitia force akaunti mwaka 2020 kwa gharama ya shilingi bilioni 2.914,tumeokoa shilingi milioni 85  ambazo zimetumika  kununua kiti na meza kwa kila mtumishi,kutengeneza mifereji na kutengeneza sakafu ya tofali za saruji maeneo yote yanayozunguka jengo’’,alisema Mpenda.

Amesema kupitia fedha zilizobakia Halmashauri pia imeweza kununua  kwa ajili ya ukumbi wa mikutano vikiwemo viti,meza vifaa, vipaza sauti na  vifaa vya kuzungumzia(Microphone).

Mkurugenzi huyo Mtendaji wa Halmashauri ya Madaba ameutaja mradi mwingine ambao unatekelezwa na Halmashauri hiyo hivi sasa ni ujenzi wa nyumba saba za watumishi ambapo serikali imetoa shilingi milioni 600 kutekeleza mradi huo.

Amesema kati ya fedha hizo shilingi milioni 300 zimetengwa kwa ajili ya kujenga nyumba ya ghorofa moja ya kuishi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo na shilingi milioni 300 zimetengwa kwa ajili ya  kujenga nyumba sita za wakuu wa Idara.

Kwa mujibu wa Mpenda kila nyumba ya Mkuu wa Idara inagharimu shilingi milioni 50 na kwamba mradi huo unatekelezwa kwa mfumo wa force akaunti ambapo hadi sasa mradi umefikia hatua nzuri,na unatarajia kukamilika Mei 2021.

“Tunaishukuru sana serikali kupitia Rais wetu Dkt.John Magufuli kwa kweli sisi Halmashauri ya Madaba tumepewa upendeleo wa kipekee nadhani ni kwa sababu Halmashauri yetu bado changa hivyo kuna uhitaji mkubwa wa kuwa na miundombinu mbalimbali’’,alisema Mpenda.

Halmashauri ya Madaba ni miongoni mwa Halmashauri tatu zilizopo katika Wilaya ya Songea,Halmashauri nyingine ni Manispaa ya Songea na Halmashauri ya Songea.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Machi 9,2021

 

  •  

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.