• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa bilioni 60 kuanza ujenzi barabara ya lami Likuyufusi-Mkenda

Imewekwa kuanzia tarehe: January 17th, 2023

SERIKALI ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imetoa shilingi bilioni 60 kuanza ujenzi barabara ya lami kilometa 60 kutoka Likuyufusi  Kwenda Mkenda Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.

Barabara hiyo ni ya mpakani mwa Tanzania na Msumbiji yenye urefu wa kilometa 124 ambayo ina Kwenda hadi katika daraja la Mkenda Mto Ruvuma mpakani mwa Tanzania na Msumbiji.

Meneja wa TANROADS Mkoa wa Ruvuma Mhandisi  Ephatar Mlavi amesema serikali kwa kuanzia inatekeleza mradi huo kwa kilometa 60  kuanzia  Likuyufusi Manispaa ya Songea hadi Mkayukayu Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

“Mradi huu utahusisha ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami, sehemu ya Likuyufusi – Mkayukayu yenye urefu wa kilometa 60’’,alisema Mhandisi Mlavi.

Hata hivyo amesema Zabuni ya mradi huo imeshatangazwa na imefunguliwa kuanzia Januari 2023 na kwamba utekelezaji wa mradi huo unatarajiwa kuanza wakati wowote baada ya hatua stahiki za manunuzi kukamilika.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Songea Mheshimiwa Pololet Mgema kwa niaba ya wananchi wa wilaya hiyo,amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za kutekeleza mradi huo  ambao unaunganisha Tanzania na Msumbiji kwa barabara ya lami.

Amesema barabara hiyo itafungua fursa za biashara na uwekezaji kwa nchi mbili za Tanzania na Msumbiji  na kwamba wafanyabiashara na wawekezaji wataweza Kwenda katika nchi hizo kuangalia fursa mbalimbali zilizopo.

Baadhi ya wananchi wanaoishi kando kando mwa barabara hiyo wamesema kwa miaka mingi barabara hiyo  katika sekta ya usafiri na usafirishaji imekuwa kero kubwa hasa wakati wa masika kutokana na ubovu wa barabara.

Kwirinus Mapunda Mkazi wa Litapwasi amesema wananchi wanatarajia makubwa mradi huo utakapokamilika kwa sababu vyombo vya usafiri vitaongezeka hivyo kupunguza gharama za usafiri.

Amesema katika eneo la Muhukuru  kuna mgodi wa makaa ya mawe ambao Mwekezaji alishindwa kufanya kazi ya kuingiza magari ya kubeba makaa ya mawe kutokana na ubovu wa barabara hivyo amesema barabara hiyo ikiwekwa lami itaongeza wawekezaji ambao pia wataongeza ajira kwa wananchi.

Serikali imetenga shilingi bilioni 46.35 kwa ajili ya kuboresha sekta ya barabara mkoani Ruvuma katika bajeti ya  mwaka 2022/2023 .

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Januari 17, 2023

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.