• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa bilioni saba kutekeleza miradi ya maji Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: March 13th, 2021

SERIKALI ya Awamu ya Tano imetoa zaidi ya shilingi bilioni saba kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya Maji Mkoani Ruvuma.

Akizungumza na wanahabari ofisini kwake mjini Songea,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme  amesema fedha hizo ni kwaajili ya miradi ya Wilaya za Songea,Mbinga na Tunduru.

“ Tunapokwenda kuadhimisha wiki ya Maji kuanzia Machi 16 hadi 22 sekta ya maji imefanya kazi kubwa sana ya kutekeleza kwa vitendo kaulimbiu ya kumtua mama  ndoo maji kichwani’’,alsema Mndeme.

Amesema kupitia Wakala wa Maji Vijijini RUWASA  NA Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira SOUWASA,kazi kubwa imefanyika ambapo serikali  imetoa zaidi ya shilingi bilioni 7 kwaajili ya uwekezaji wa maji ndani ya Mkoa wa Ruvuma.

 Hata hivyo amesema hadi sasa fedha iliyopokelewa ni zaidi ya shilingi bilioni tano na kwamba kiwango cha usambazaji wa maji safi wilaya ya Songea kimeweza  kuongezeka kutoka asilimia 74 hadi asilimia 86.2.

Kwa mujibu wa Mndeme wilaya ya Mbinga imepokea zaidi ya shilingi bilioni moja na kwamba huduma ya maji imeongezeka kutoka asilimia 52.2 hadi asilimia 70.8 na wilaya ya Tunduru imepokea fedha zaidi ya shilingi milioni 600 na kiwango cha usambazaji maji kimeongezeka kutoka asilimia 55 hadi 66.

Hata hivyo Mndeme amesema licha ya mafanikio hayo kuna changamoto za vyanzo vya maji katika Manispaa ya Songea ambazo zinasababisha upungufu wa maji kutoakana na ongezeko kubwa la idadi ya watu  na mahitaji ya Maji yanaongezeka.

Amesema katika kukabiliana na changamoto hizo,Mkoa kupitia SOUWASA umefanya juhudi mbalimbali za kukabiliana na changamoto hizo ikiwemo kuhakikisha mtandao wa mabomba unawafikia  watumiaji maji kikamilifu.

Mndeme amewapongeza RUWASA Mkoa wa Ruvuma  kwa kupambana na kuhakikisha Maji yanapatikana Mijini na Vijijini katika Mkoa wa Ruvuma unakadiriwa kuwa wakazi    zaidi ya milioni  1.34.

Kwa upande wake Meneja wa RUWASA Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Rebman Ganshonga amesema katika kipindi cha kuanzia Julai mwaka  2019 hadi Februari 2021  RUWASA  Ruvuma imepokea zaidi ya shilingi bilioni 20 kutoka serikali kuu katika kutekeleza uboreshaji miradi ya maji.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Machi 13,2021.

 

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.