• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa pikipiki kwa maafisa watendaji Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: March 2nd, 2023

SERIKALI kupitia TAMISEMI imetoa pikipiki kwa ajili ya maafisa watendaji kata katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.

Akikabidhi pikipiki hizo kwa watendaji wa kata ,Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma  Mheshimiwa Ngollo Ng’waniduhu Malenya  aliwaambia watendaji wa kata hao kuwa Serikali imedhamiria kuwahudumia wananchi kwa kuwapatia watendaji wa kata pikipiki ili kurahisisha usafiri wa kuwafikia wananchi kiurahisi.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Malenya alidai ipo mifano  katika mikoa mingine  watendaji wa kata waliopatiwa pikipiki kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wanatumia pikipiki hizo tofauti na malengo ya serikali.

Malenya  aliwataka watendaji wa kata waliopatiwa pikipiki hizo kufanyia kazi za serikali kama ilivyokusudiwa na kinyume cha hapo serikali ya wilaya itafuatilia kwa makini kuhakikisha pikipiki hizo zinafanya kazi ya kusafiria  kwenda kutatua kero za wananchi na kusimamia shughuli za maendeleo katika kata zao.

Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo  Paul Ambokile  alimwambia mkuu wa wilaya  kuwa, kata zilizopendekezwa kupata pikipiki hizo ni kata ya magazine,kata ya Lusewa,Kata ya Msisima ,Lisimonji,Mputa pamoja na kata ya Kitanda.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Kassimu Gunda aliwahatarisha watendaji wa kata kuwa wasitumie pikipiki hizo kusafirisha nyumba ndogo kwa kuwatumia vijana hali ambayo itasababisha ndoa zao kugundua kuwa pikipiki hizo ndio chanzo cha maovu na kuibua hasira za kukata matairi ya pikipiki hizo na kusimamisha shughuli za kutatua kero za wananchi na kusimamia shughuli za maendeleo.

Gunda Alisema madiwani  watafuatilia katika kata zao kuhakikisha pikipiki hizo zilizotolewa na serikali na kupewa watendaji wa kata zinafanya kazi zilizokusudiwa na sio vinginevyo alisema makamu mwenyekiti huyo.

Ambokile aliongeza kuwa sababu ya kupendekezwa kwa kata hizo ni kutokana na changamoto za miundombinu ya barabara  zilizopo katika kata hizo ,katika kuwafikia wananchi wa vijiji vya kata  na kuwarahihishia watendaji wa kata kutembelea  vijiji na kusimamia shughuli za maendeleo.

Mtendaji wa kata ya Magazini Musa Ponera pamoja na kuishukuru Serikali kwa kumpatia pikipiki hiyo alisema kata ya magazine ipo umbali wa zaidi ya kilomita 200 kutoka makao makuu ya Halmashauri ,kupewa kwa pikipiki hiyo imemrahihishia usafiri wa kufika makao makuu ya Halmashauri kwa shughuli za kikazi pamoja na kutembelea vijiji vya kata yake kutatua kero za wananchi na kusimamia maendeleo na kuhaidi kuitunza pikipiki hiyo ili aweze kufanyakazi iliyokusudiwa na serikali alisema Ponera

Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo ina jumla ya kata 21 ambapo kata 6 kati ya hizo zimepata pikipiki katika mgao huu wa awamu ya kwanza na kubakia kata 15 ambazo watendaji wake watapata katika awamu zijazo .

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.