• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa shilingi milioni 460 kujenga lami barabara ya Longa-Litoho Mbinga

Imewekwa kuanzia tarehe: March 15th, 2023

SERIKALI kupitia wakala wa barabara za vijijini na mijini(Tarura),imeanza awamu ya kwanza ya ujenzi  mradi wa barabara ya Longa- Kipololo-Litoho wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma yenye urefu wa km 1 kwa kiwango cha lami kwa gharama ya shilingi milioni 460.

Meneja wa TARURA wilaya ya Mbinga Mhandisi Oscar Mussa amesema,katika ujenzi wa barabara hiyo kazi zilizofanyika ni ujenzi wa tabaka mbili za lami,kujenga mitaro mita 300 na kufunga taa kumi za barabarani katika maeneo tofauti.

Aidha alisema,katika barabara hiyo wamejenga kipande kingine cha chenye urefu wa kilomita  25 kwa kiwango cha changarawe,na kuziba mashimo kwa gharama ya shilingi milioni 250.

Mhandisi Mussa alisema,mradi huo umetekelezwa na mkandarasi wa ndani kampuni ya Ovans Construction Ltd  na ulianza kutekelezwa mwezi Agosti na kukamilika mwezi Disemba 2022,na sasa mkandarasi anakamilisha ujenzi wa mitaro.

Alisema,barabara hiyo ni muhimu sana kiuchumi kutokana na wananchi wengi wa maeneo hayo kuwa wazalishaji wakubwa wa mazao ya chakula na biashara hasa mahindi,kahawa na maharage ambapo sasa wataweza kusafirisha mazao yao kwenda sokoni kwa urahisi.

Mussa aliongeza kuwa,kujengwa kwa  barabara hiyo kwa kiwango cha lami na kuboreshwa  kwa kiwango cha changarawe itarahisisha na kurudisha mawasiliano kati ya wilaya ya Mbinga na Nyasa  na kufupisha safari kwa wananchi wa wilaya hizo mbili.

Amewataka wananchi kuhakikisha wanatunza barabara hiyo na miundombinu yake, ili iweze kudumu kwa muda mrefu na iwasaidie katika shughuli zao za maendeleo kwa sababu fedha zilizotumika kufanikisha ujenzi  huo zimetokana na kodi zao.

Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Litoho wilayani humo,wameshukuru kujengewa barabara hiyo kwa kiwango cha lami kwani kwa muda mrefu walipata mateso makubwa pindi wanaposafiri kwenda Mbinga mjini ambapo walitumia kati ya masaa 4 hadi 6 na sasa  wanatumia muda wa saa 1.

Hata hivyo Mapunda,ameiomba serikali kumalizia kipande kilichobaki cha barabara kujenga kwa lami badala ya changarawe,ili kuunganisha barabara mawasiliano kati ya wilaya ya Mbinga na Nyasa.

Gallus Hyera mkazi wa kijiji cha Ulima kata ya Ukata wilayani Mbinga alisema,kabla ya kujengwa kwa barabara hiyo kwa kiwango cha lami hali ya mawasiliano ilikuwa mbaya sana kwani wakati wa masika walilazimika kulala barabara kutokana na magari waliyokuwa wanasafiri nayo kukwama barabarani.Alieleza kuwa,hali hiyo imechelewesha  saa maendeleo ya wananchi wa maeneo hayo licha ya kazi kubwa wanazozifanya za uzalishaji mkubwa wa mazao ya chakula na biashara.

Hyera,amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kutoa fedha ambazo zimewezesha kujengwa kwa  barabara hiyo  kwa kiwango cha lami na kuipongeza Tarura kwa kusimamia

ujenzi wa mradi huo muhimu  kwa uchumi wa wilaya ya Mbinga.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.