• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa zaidi ya shilingi bilioni 93 kuboresha bandari za ziwa Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: May 6th, 2025

Serikali ya Awamu ya Sita imewekeza shilingi bilioni 93.2 kuboresha miundombinu ya bandari katika Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma, hatua inayolenga kuimarisha usafiri wa majini na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika ukanda wa Ziwa Nyasa.

Uwekezaji huo umehusisha ujenzi wa bandari mpya ya Ndumbi kwa gharama ya shilingi bilioni 12.2, ambayo imekamilika na tayari imeanza kutoa huduma. Aidha, serikali imetenga shilingi bilioni 81 kwa ajili ya ujenzi wa bandari ya kisasa ya Mbambabay unaotarajiwa kukamilika Januari 26, 2026.

Mbunge wa Jimbo la Nyasa, Mhandisi Stella Manyanya, amesema kuwa bandari ya Ndumbi imekamilika kwa asilimia 100 na inahudumia abiria na mizigo kwa ufanisi mkubwa. Meneja wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari za Ziwa Nyasa, Manga Gassaya, amesema bandari hiyo sasa ina uwezo wa kuhudumia mizigo ya hadi tani 110,000 kwa mwaka, kutoka tani 76,000 za awali, na abiria kutoka 56,000 hadi 126,000 kwa mwaka.

“Hii ni hatua kubwa katika kufungua usafirishaji wa ndani na nje ya nchi kupitia Ziwa Nyasa,” amesema Gassaya.

Kuhusu mradi wa bandari ya Mbambabay, Kaimu Mhandisi wa TPA, Fabian Paul, amesema bandari hiyo itakuwa na uwezo wa kupokea meli mbili zenye uzito wa tani 5,000 kila moja, jengo la utawala, ghala la kuhifadhi mizigo, nyumba za wafanyakazi na eneo la kuhudumia mizigo la mita za mraba 20,000.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, akizungumza alipotembelea kukagua mradi huo,alisema kukamilika kwa bandari hiyo kutaimarisha uchumi wa Mkoa wa Ruvuma na mahusiano ya kibiashara na nchi jirani za Malawi na Msumbiji.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.