• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa zaidi ya shilingi bilioni 244 kutekeleza miradi ya maendeleo Tunduru

Imewekwa kuanzia tarehe: August 22nd, 2024

Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan  katika kipindi cha miaka miwili imetoa Zaidi ya shilingi bilioni 244 kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani Tunduru.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed wakati anazungumza na wananchi wa Tunduru kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja  vya Baraza la Eid mjini Tunduru.

Amesema fedha hizo zinaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika Wilaya hiyo ikiwemo miradi katika sekta ya elimu ambapo hivi sasa katika wilaya hiyo wanafunzi wote wanaofaulu kujiunga na kidato cha kwanza wanachaguliwa kwa kuwa Wilaya ina miundombinu ya vyumba vya madarasa vya kutosha.

“Kwenye sekta ya afya napo tumepiga hatua kubwa kwani wananchi wetu wanapata huduma ya afya vizuri katika hospitali ya Wilaya,vituo  vya afya  na zahanati zetu kwa ukaribu zaidi’’,alisisitiza.

Akizungumzia sekta ya kilimo,Kanali Abbas amesema  serikali imeimairisha mfumo wa stakabadhi za ghala ambapo wakulima wanauza mazao yao kwa bei ambayo inamwezesha mkulima kurudisha gharama zake anazozitumia katika uzalishaji.

Hata hivyo amesema karibu sekta zote zikiwemo za umeme,maji,barabara za vijijini na mjini zinafanya vizuri kutokana na serikali kutoa fedha za kutekeleza miradi hiyo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Dr.Wilfred Rwechungura  amesema Halmashauri hiyo inaendelea kufanya jitihada mbalimbali za kukabiliana na upungufu wa madarasa ,madawati,viti na meza za wanafunzi.

Hata hivyo amesema hadi sasa katika shule za sekondari Halmashauri haina upungufu wa vyumba vya madarasa,viti na meza,badala yake kuna upungufu wa madarasa na madawati katika shule za msingi.

Rwechungura amesema katika kukabiliana na changamoto hiyo,Halmashauri ya Wilaya imekuwa inatenga fedha kutoka vyanzo vya ndani na serikali kuu ili kujenga miundombinu ya shule ambapo kuanzia mwaka 2021 zaidi ya shilingi bilioni 2.5 zimetumika kujenga madarasa katika shule za msingi.

Kaimu Mkurugenzi huyo amesema kupitia mradi wa BOOST Halmashauri hiyo imeweza kupokea zaidi ya shilingi bilioni 1.2 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika shule za msingi.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma anafanya ziara ya kikazi katika Halmashauri zote nane za Mkoa wa Ruvuma kwa lengo kuzungumza na wananchi ,kusikiliza kero zao na kupashana Habari za maendeleo zinazofanywa na serikali ikiwemo utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.