• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatumia bilioni 7.7 kujenga sekondari za mfano 11 Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: November 27th, 2022

SERIKALI ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imejenga shule mpya 11 za sekondari mkoani Ruvuma zilizogharimu shilingi bilioni 7.7.

Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Mipango  katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Jumanne Mwankoo amezitaja shule hizo mpya kuwa  zimejengwa katika Halmashauri zote nane za Mkoa wa Ruvuma.

Amesema shule hizo zimejengwa kupitia mradi wa kuboresha Elimu ya Sekondari nchini (SEQUIP) ambapo kila Halmashauri imejengwa shule moja kwa thamani ya shilingi milioni 470.

Hata hivyo amesema katika Halmashauri ya Tunduru zimejengwa shule tatu za sekondari kupitia mradi wa SEQUIP na kwamba katika Halmashari ya Namtumbo pia zimejengwa shule mbili ikiwemo shule ya wasichana ya Mkoa iliyojengwa katika eneo la Migelegele kwa gharama ya shilingi bilioni  tatu.

“Mradi wa SEQUIP umewezesha kila shule ya sekondari kuwa na jengo la utawala,vyumba vya madarasa, vyoo,mfumo wa maji, maabara,maktaba na jengo la TEHAMA ,shule zote zinatarajia kuanza kuchukua wanafunzi Januari 2023’’,alisema.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amekagua moja ya shule hizo katika Halmashauri ya Madaba.

Akitoa taarifa ya mradi wa shule hiyo kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Madaba Sajidu Idrisa Mohamed amesema mradi wa ujenzi  umetengewa shilingi milioni 470 na ulianza utekelezaji Machi 2022 ambapo hadi sasa fedha zilizotumika ni zaidi ya shilingi milioni 468.

Amesema ujenzi wa mradi huo upo katika hatua za ukamilishaji ambapo hadi sasa umefikia asilimia 95 ukihusisha ujenzi wa madarasa nane,jengo moja la utawala,vyumba vitatu vya maabara,matundu 20 ya vyoo,minara miwili ya matanki na mfumo wa kunawa mikono.

Hata hivyo amesema ujenzi upo katika asilimia 65 kwa majengo mawili ambayo ni jengo la  maktaba na chumba cha TEHAMA na kwamba mradi unatarajia kukamilika kwa asilimia 100 kabla ya mwisho wa mwaka huu.

Akizungumza mara baada ya kukagua mradi huo,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amemwagiza Mkandarasi kushughulikia dosari zote zilizojitokeza ikiwemo mipasuko kwenye kuta.

Amesema Rais ametoa fedha nyingi kutekeleza mradi huo hivyo ni lazima majengo yalingane na thamani ya fedha kwa kutekeleza mradi katika ubora na viwango.

Katibu Tawala wilaya ya Songea Pendo Ndumbaro ameahidi maagizo yote yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa kuyafanyia kazi ambapo amemwagiza Mkandarasi kufanya kazi usiku na mchana ili kukamlisha mradi huo.

Serikali inatekeleza mradi wa Kuboresha Elimu ya Sekondari (SEQUIP) kwa kujenga shule mpya za sekondari 1000 katika nchi nzima.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Novemba 27,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.