• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SHAMBA la NAFCO Namtumbo kutumika kuzalisha mbegu za serikali

Imewekwa kuanzia tarehe: December 2nd, 2022

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas ameagiza hekta 3500 zilizopo katika Shamba la NAFCO Namtumbo zitumiwe na Wakala wa Mbegu Tanzania ASA kuzalisha mbegu za serikali.

Ametoa agizo hilo katika kikao klichofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo kilichowakutanisha Wakala wa Mbegu Tanzania (ASA),watalaam kutoka Halmashauri ya Namtumbo,Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na Wilaya ya Namtumbo.

Hata hivyo amesema shamba lililokuwa na NAFCO Namtumbo ambalo Hazina imelikabidhi kwa ASA lina jumla ya hekta 5000 na kwamba hekta 1500 wameachiwa wananchi wa vijiji vya Suluti na Migelegele ili waweze kulima mazao mbalimbali.

“Nakuagiza Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo hakikisha wananchi wanasomewa hii barua kwamba shamba zima la NAFCO Namtumbo Hazina imelikabidhi rasmi kwa ASA,ili wananchi wajue mapema wasiingie kwenye mgogoro’’,alisisitiza Kanali Thomas.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma pia ameagiza shamba hilo litumike kuongeza mbegu za serikali hasa alizeti,ufuta na soya na mazao mengine yanayokubali katika ukanda za kusini.

Akizungumza kwenye kikao hicho Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mbegu Tanzania (ASA) Dkt.Sophia Kashenge  alisema serikali imeanisha shamba la NAFCO Namtumbo lenye ukubwa  hekta 5000 liweze kutumika kuzalisha mbegu ili kuongeza uzalishaji wa mbegu nchini.

Amesema kikao kilichofanyika kati ya Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kimemaliza changamoto zilizojitokeza wakati wa uanishaji wa  maeneo ya shamba hilo.

Hata hivyo  Dkt.Kashenge amesema maelekezo ya Waziri wa Kilimo yalikuwa ni shamba la NAFCO Namtumbo litumike kuzalisha mbegu za serikali ili kukidhi mahitaji ya mbegu bora nchini.

Amesema  serikali ilikuwa haina shamba la mbegu  katika Kanda ya Kusini hivyo amesisitiza kuwa shamba hilo kwa upande wa serikali lina umuhimu mkubwa kwa ikolojia ya Kusini.

Amesisitiza kuwa serikali imeamua kuchukua shamba la NAFCO Namtumbo kama ilivyochukua shamba la NAFCO Mbozi ambalo hivi sasa lina  jumla ya Kampuni nane zinazozalisha  zaidi ya tani 7,000 za Mbegu.

Amesema shamba la NAFCO Namtumbo likitumika vizuri litaongeza mchango wa uzalishaji wa mbegu za serikali nchini.

Shamba la NAFCO Namtumbo lilikuwa chini ya Hazina,ambapo Msajiri wa Hazina amelikabidhi rasmi shamba hilo kwa Wakala wa Mbegu Tanzania(ASA).

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Desemba 2,2022


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.