• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SH.Bilioni 1.3 zilizvyomaliza kero ya maji Ruvuma chini

Imewekwa kuanzia tarehe: October 25th, 2022

WAKAZI wa kijiji cha Ruvumachini Halmashauri ya mji Mbinga mkoani Ruvuma,wameishukuru serikali kwa kuanza ujenzi wa mradi mkubwa wa maji  unaokwenda kumaliza kero ya muda mrefu ya maji  safi na salama katika kijiji hicho.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti mbele ya Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas walisema, tangu Serikali  ilipoanza kujenga  mradi huo wana matumaini makubwa ya kuishi na kuwa na maisha bora na kuondokana na tabu na mateso makubwa yanayo sababishwa na ukosefu wa maji ya bomba.

Akiongea kwa niaba ya wenzake Hagapi Komba alisema,changamoto ya maji katika kijiji hicho ni kubwa na ya muda mrefu hali iliyosababisha baadhi ya watumishi wa serikali wanaopelekwa kufanya kazi wakiwamo walimu wa shule ya msingi kuomba uhamisho kwenda shule nyingine na wengine kukimbia ili kuepuka kero ya maji.

Aidha alieleza kuwa,hata wanafunzi wanalazimika kwenda shule wakiwa wachafu,hivyo kusababisha kufanya vibaya katika masomo yao  na kuiomba serikali kukamilisha mradi huo haraka.

Diwani wa kata ya Mpepai Donalt Mbepera, ameipongeza serikali kupitia wakala wa maji safi na salama vijijini(Ruwasa)mkoa waRuvuma kwa kuona umuhimu wa kujenga mradi huo ambao utahudumia wananchi wa kijiji hicho na vijiji vingine vinavyounda kata ya Mpepai.

Mbunge wa Jimbo la Mbinga mjini Jonas Mbunda,amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anayofanya kuhakikisha wananchi wa jimbo hilo wana kuwa na maisha bora kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali.

Mbunda alisema, uamuzi wa serikali  kutoa kiasi cha Sh.bilioni 1.3 kwa ajili ya kutekeleza mradi huo  imethibitisha uaminifu wake kwa wananchi wa jimbo hilo na kudhihirisha  kauli mbiu ya kumtua mama ndoo kichwani.

Amewaomba wananchi wa Ruvumachini na jimbo lote la Mbinga Mjini,kuhakikisha wanakuwa walinzi wa mradi huo na miradi mingine inayotekelezwa katika vijiji mbalimbali yenye lengo la kuleta maendeleo na kuboresha maisha yao.

Naye Mkuu wa mkoa huo Kanali Laban Thomas,ameuagiza uongozi wa wakala wa maji safi na usafi  wa mazingira(Ruwasa) mkoa wa Ruvuma, kuhakikisha inamsimamia mkandarasi anayejenga mradi huo kampuni ya Nipo Africa Engineering ili akamilishe kazi kwa wakati na ubora wa hali ya juu.

Kanal Laban,amewataka wananchi wa kijiji cha Ruvuma chini,kutunza mradi huo pamoja na vyanzo vya maji na kuacha kufanya shughuli yoyote kwenye maeneo yaliyotengwa mahususi kwa ajili ya manufaa ya kizazi cha sasa na baadaye.

Alisema,serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan inafanya jitihada kubwa za kutafuta fedha ili kuboresha maisha ya wananchi wake,hata hivyo haitakuwa na maana iwapo miradi  hiyo itahujumiwa  na kutotaleta tija iliyokusudiwa.

Mkuu wa mkoa,amewakumbusha viongozi wa serikali ya kijiji na kata, kuhusu wajibu wao katika kusimamia vyanzo vya maji na kutumia sheria zilizopo kuwachukulia hatua watu wanaoharibu kwa makusudi vyanzo hivyo na miradi yote ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao.

Awali meneja wa Ruvuma wilaya ya Mbinga Mashaka Sinkara alisema,mradi wa maji wa Ruvuma chini ulianza kutekelezwa mwezi  Machi mwaka huu na unatarajiwa kukamilika mwezi Novemba.

Alisema,muda wa utekelezaji wa mradi huo ni miezi sita ambapo hadi sasa umefikia asilimia sitini na serikali imetenga  Sh.bilioni 1.3 kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo na unatarajiwa kuwanufaisha wakazi zaidi ya elfu moja.


Katika hatua nyingine Sinkara alieleza kuwa, serikali imetoa jumla ya Sh.bilioni 1.3 kwa ajili ya kujenga mradi  mwingine wa maji Mbangamao  kijiji cha Mbangamao chenye wakazi wapatao  elfu mbili na mia tisa.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.