• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SHIRIKA la Compassion Tanzania linavyohudumia watoto 4200 Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: July 7th, 2022

SHIRIKA la Kikristo la Compassion International Tanzania (CIT) lililojikita kuwasaidia Watoto wanaotoka kaya masikini limeweza kuwahudumia Watoto 4200 katika Mkoa wa Ruvuma.

Hayo yamesema na Mkurugenzi wa CIT nchini Mary Lema wakati anazungumza kwenye uzinduzi wa kampeni  ya ulinzi wa mtoto  iliyofanyika katika  viwanja vya kanisa la Anglikana Kijiji cha Mkongo wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma.

Lema amesema Shirika la CIT liliingia mkoani Ruvuma mwaka 2019 na kuanza kutoa fedha za ufadhili kwa Watoto kutoka kaya masikini Machi mwaka 2020.

“Matokeo ya huduma hii yamekuwa Dhahiri kwa ukubwa wake kwa Watoto walengwa,walezi,kaya na jamii kwa ujumla, kwa kushirikiana na makanisa,tumeweza kuboresha mazingira ya elimu kwa Watoto kwa kuhakikisha wanapata mahitaji wezeshi kama vitabu,sare za shule na kutoa Bima ya afya’’,alisisitiza Mkurugenzi wa CIT.

Hata hivyo amesema Shirika la CIT kwa kushirikiana na makanisa wenza, wanaweza kuhudumia Watoto na vijana katika Nyanja mbalimbali za Maisha huku mkazo mkubwa ukiwekwa kisera na kivitendo ili kuhakikisha mtoto analindwa dhidi ya vitendo vya unyanyasaji.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa CIT,Shirika hilo lilianza kufanya kazi hapa nchini mwaka 1999 jijini Arusha ambapo hivi sasa linafanya kazi katika mikoa 21 na wilaya 80 na kwamba hadi sasa limefadhili Watoto na vijana walengwa Zaidi ya 112,000 kupitia makanisa washirika Zaidi ya 503.

Mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo,Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri  ya Wilaya ya Namtumbo Godwin Rutta amelipongeza Shirika hilo kwa kazi kubwa inayoendelea kufanywa kwa wananchi bila ubaguzi wowote.

Amesema serikali inatambua mchango huo na ipo tayari wakati wowote kushirikiana na makanisa ili kuhakikisha nia njema iliyokusudiwa ya kuboresha maisha inawafikia wananchi.

Ametoa rai kwa wananchi wa madhehebu yote wilayani humo kuhakikisha wanawapeleka Watoto wao kupata elimu katika shule inayomilikiwa na kanisa la Anglikana ili kuwajengea Watoto wao msingi wa elimu.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo Naibu Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Ruvuma padre Martin Mande amelipongeza Shirika la CIT kwa kusaidia huduma ya mtoto katika kanisa hilo.

“CIT mmetufanya kanisa lionekane linafanya kazi yake kimwili na kiroho kwa ufanisi mkubwa,mmetembelea Ruvuma na kufika hapa Mkongo kwenye kituo cha Anglikana sisi hatukuwa hivi tunawashukuru sana’’,alisisitiza Naibu Askofu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Elimu wa Kanisa Anglikana Dayosisi ya Ruvuma,Padre John Midelo  amesema mradi huo umeweza kumkomboa mtoto katika umasikini.

Hata hivyo amesema mradi unatekelezwa katika makanisa yaliyopo wilaya za Namtumbo,Tunduru na Songea wanufaika wakubwa ni Watoto na vijana wanaotoka katika kaya masikini.

Amesema katika kipindi cha miaka mitatu  kanisa la serikali wamenufaika kupitia mradi huo ambapo kanisa Anglikana pekee limeajiri vijana 23 na Watoto wengi wakinufaika na uwepo wa shule zinazoendeshwa kupitia mradi huu ambapo katika kituo cha Mkongo wanatarajia kukamilisha usajiri wa shule hiyo hivi karibuni.

Imeandikwa na Albano Midelo

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Julai 7,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.