• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SIMBA,CHUI NA MAMBA kuongezwa katika bustani ya wanyamapori Luhira

Imewekwa kuanzia tarehe: December 9th, 2022


SERIKALI kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii  inatarajia kuongeza Wanyama jamii ya simba, chui, fisi,mbuni,kobe na mamba katika bustani ya wanyamapori Luhira Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma 

Antony Masebe ni Kamanda wa  Kituo Kidogo cha Kanda Kusini Mashariki amesema utengenezaji wa vibanda maalum vya kuwahifadhi Wanyama hao (cages) unaogharimu shilingi milioni 78 unaendelea katika bustani ya Luhira.

Masebe amesema serikali pia imetoa shilingi milioni 103 kujenga ukumbi wa kisasa katika bustani hiyo na vibanda viwili vya kupumzikia ambavyo vimegharimu shilingi milioni 20.

Amesema kituo hicho ambacho kipo chini ya TAWA kinasimamia bustani ya asili ya Luhira ambayo ilianzishwa mwaka 1973 na imekuwa inapokea watalii wa aina mbalimbali kutoka ndani ya nje ya nchi.

“Bustani ya Luhira imekuwa inatoa elimu na kuwasaidia wanafunzi kuanzia shule za msingi,sekondari na vyuo kuweza kujipatia maarifa tofauti kuhusu utalii ’’,alisisitiza Masebe.

Daudi Tesha ni Afisa Mhifadhi katika Bustani ya Luhira ameitaja bustani  hiyo kuwa ndiyo bustani pekee Tanzania yenye uoto wa asili ikiwa na ukubwa wa hekta 600 ipo umbali wa kilometa saba kutoka mjini Songea.

Amewataja Wanyama ambao wanapatikana katika bustani hiyo kuwa ni pundamilia, pofu, kakakuona, kuro, swalapala, sungura,nyumbu,jamii ya nyani ambapo amesema bustani hiyo ina madhari ya kuvutia ikiwemo maeneo ya michezo ya Watoto,maeneo mazuri ya kupigia picha na kuweka kambi kwa ajili ya utafiti.

Amekitaja kiingilio cha bustani hiyo kuwa ni shilingi 2,360 kwa mtu  wa kuanzia umri wa miaka 18,chini ya miaka 17 ni shilingi 1180 na  kwa Watoto chini ya miaka mitano wanaingia bure hivyo ametoa rai kwa wakazi wa Mkoa wa Ruvuma na watanzania wote kutembelea bustani hiyo asili.

Amesema bustani ya Luhira imeweka mkakati wa kuwa na aina mbili za makazi ya Wanyama wakiwemo Wanyama huru kama pundamilia na pofu na kwamba hivi sasa wanatarajia kuongeza Wanyama wanaishi kwenye vizuizi yaani cages  ambapo mpango uliopo ni kuleta Wanyama wanaovutia wengi kama mfalme wa msituni  simba na chui.

“Hifadhi ya Luhira ina eneo kubwa, ambalo linahitaji uwekezaji mkubwa,tunafikiria kuwaleta wanyama wakubwa kama  simba na kuongeza maeneo ya kuvutia wageni wanapokuwa ndani ya bustani ya Luhira’’,alisisitiza Tesha.

Ameitaja mikakati mingine ya kuboresha bustani hiyo kuwa ni kuanzisha michezo ya kutekeleza kwenye waya (Zipline) kama inavyofanyika katika nchi ya Afrika ya Kusini,kuweka bwawa la kisasa la kuogelea na kuboresha eneo maalum la kupigia picha.

Amesema baada ya kuoresha bustani hiyo na kuongeza vivuito wanatarajia pia idadi ya watalii kutoka ndani na nje pia itaongezeka.

Ametoa rai kwa wakazi wa Mkoa wa Ruvuma na mikoa ya kusini kufika katika hifadhi ya Luhira kujionea fursa za utalii zilizopo katika hifadhi hiyo  pekee ya asili nchini Tanzania iliyopo mjini Songea.

Tesha amesisitiza kuwa hifadhi ya Luhira ni eneo la asili lenye utajiri wa miti ya miyombo, misuku, mitumbitumbi, miwanga, minyonyo, mizambarau, mininga, na mikuyu,na kwamba ni miongoni mwa bustani chache zenye uoto wa asili kabisa zilizopo mjini.

Amesema ndani ya Luhira,mtalii anaweza kufanya utalii wa kutembea kwa miguu,kupiga picha,kuangalia wanyama na ndege,utalii wa kuweka kambi(camping) na kwamba mapumziko ya mchana(picnic) hufanyika ndani ya eneo maalum katika bustani hiyo.

“Watalii kutoka nje ya nchi pia wanatembelea hifadhi yetu, tumepokea watalii toka Ujerumani,Afrika ya Kusini, India, Marekani, Ufaransa,Italia, Uholanzi na wageni toka mikoa mbalimbali nchini,wanafanya utalii wa kuchunguza aina ya mimea na ndege’’,alisema Tesha.

Hifadhi ya asili ya Ruhila,inafikika kwa urahisi kwa ndege au kutumia barabara ya Njombe hadi Songea,Mtwara hadi Songea ambayo ni ya lami.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Desemba 9,2022

 

 

           

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI Mwenge wa uhuru ashiriki upandaji miti Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru waweka jiwe la msingi shule ya amali Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru wazindua jengo la EMD Peramiho

    May 10, 2025
  • MWENGE wa uhuru waingia Pers

    May 10, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.