• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SOKO la wakulima Songea kukamilika kwa wakati

Imewekwa kuanzia tarehe: August 17th, 2022

WAFANYABIASHARA waliokuwa wanafanya shughuli zao soko la Manzese A na B  katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma,wameiomba serikali kupitia Manispaa hiyo kuharakisha ujenzi wa soko jipya ili waweze kurudi na kufanya shughuli zao kama hapo awali.

Wafanyabiashara hao wameondolewa katika soko hilo kwa ajili ya kupisha ujenzi wa  soko la kisasa litakaloendana na  hadi ya  Manispaa hiyo,kazi inayotarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia sasa.

Wakizungumza  kwa nyakati tofauti jana walisema,tangu soko hilo lilipovunjwa mwezi Julai,bado ujenzi haujaanza hivyo wana wasiwasi kazi itakuchukua muda mrefu hadi kukamilika,jambo litakalowawia vigumu kuendelea kumudu gharama ya maisha yao.

Aziz Kapakapa alisema,tangu  soko hilo  lililopo vunjwa wameathirika sana kiuchumi kwani eneo hilo ndiyo walilotegemea kupata riziki zao za kila siku,lakini kwa sasa wanaishi maisha magumu na familia zao.

Ameiomba serikali,kuharakisha kazi hiyo na kujenga soko la viwango ili kuwavutia wafanya biashara kurudi na wateja wengi kwenda kununua bidhaa zitakazopatikana katika soko hilo maarufu soko la wakulima.

Kapakapa,ameipongeza Manispaa ya Songea kuwa na mpango wa kujenga soko la kisasa,lakini ameomba imsimamie kwa karibu fundi au mkandarasi atakayepewa kazi ili  kuepuka kujengwa chini ya kiwango kwa kuwa Manispaa ya Songea ndiyo kioo kwa wageni wanafika katika mkoa wa Ruvuma.

Athuman Majimoto  mfanyabiashara  katika soko la Manzese tangu mwaka 2012 alisema, kuwaondoa katika eneo hilo ni kama uonevu kwao kwa sababu  hakuna maridhiano yoyote yaliyofikiwa kati ya Manispaa na wafanyabiashara hao.

Alisema,hawapingi kuondolewa katika eneo hilo lakini Manispaa wangetumia busara kuwashirikisha na kutoa elimu juu ya faida zitakazo patikana kutokana na  uwepo wa soko jipya.

Aidha,ameiomba Serikali mara soko litakapokamilika kuwaangalia kwanza wafanyabiashara waliokuwepo awali, badala ya kuwapa nafasi watu wenye fedha ambao hawakuwepo katika soko hilo.

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Betram Njelekela alisema,serikali imeamua kuvunja soko la Manzese A na B ili kujenga soko la kisasa katika eneo hilo, badala ya kuendelea na soko la lazima ambalo vibanda vyake viliezekwa  kwa magunia.

Alisema, mji wa Songea  unakuwa kwa kasi kubwa tofauti na miaka kumi iliyopita,na hata idadi ya watu imeongezeka sana, kwa hiyo wanahitaji vitu vizuri na siyo  kuendelea kuwa na  vitu vya kizamani na mazingira ambayo hayaendani na hadhi ya mji  maarufu wa Songea.

Alisema Manispaa ya Songea ndiyo kioo kwa mkoa wa Ruvuma,kwa hiyo ni muhimu kuwa na majengo na miundombinu ya kisasa ambayo yataendana na sifa ya mkoa huo ambao uchumi wake unakuwa kwa kasi kubwa na unaoongoza kwa uzalishaji wa chakula hapa nchini.

Amewataka wananchi hususani wafanyabiashara kuwa wavumilivu, wakati huu ambao serikali inaendelea kukamilisha taratibu za  mwisho kwa ajili ya kuanza ujenzi wa soko hilo na baada ya kukamilika  watafurahi  kutokana na uwekezaji utakaofanyika katika eneo hilo.


“kwa niaba ya mkurugenzi wa Manispaa nawaomba wananchi wa Songea watuamini kwamba sisi ni wataalam, hatufanyi vitu kwa kukurupuka hata kidogo, tunakwenda kujenga soko la kisasa ambalo baadhi yao hawajawai kuliona,nawahakikishia baada ya kukamilika hata wale wanaolalamika watafurahi na kutupongeza”alisema Njelekela.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.