• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TAASISI isiyokuwa ya kiserikali yakabidhi vyumba vya madarasa

Imewekwa kuanzia tarehe: August 18th, 2022

KATIKA kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuboresha sekta ya  elimu nchini,shirika la Tanzania Development Trust(TDT) na  Eucanaid,wamekabidhi vyumba sita vya madarasa vyenye thamani ya Sh milioni 68 kwa shule ya sekondari Mkanona Halmashauri ya wilaya Nanyumbu mkoani Mtwara.

Mbali  na vyumba vya madarasa, mashirika hayo yamekabidhi matundu  kumi  ya vyoo vya wanafunzi,choo cha walimu,ofisi ya mkuu wa shule na ofisi ya walimu wa shule hiyo ili kuwatia moyo katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku na kupunguza uhaba wa  baadhi ya miundombinu  ya shule hiyo.

Akizungumza wakati wa kukabidhi madarasa hayo mbele ya Mkuu wa wilaya ya Nanyumbo Mariam Chaurembo,mwakilishi wa TDT &UECANAID Mchungaji Linus Burian alisema,kama wadau wakubwa wa maendeleo wana wajibu wa kuunga mkono juhudi mbalimbali za serikali katika kutatua changamoto ya elimu.

Alisema, katika kata  hiyo yenye vijiji sita kwa muda mrefu hakukuwa na shule ya Sekondari na wanafunzi wanaomaliza shule ya msingi walikosa nafasi ya kujiunga na elimu ya sekondari na wachache waliopata nafasi  hiyo walilazimika kwenda kusoma shule  ya sekondari  kata  nyingine ya Nanyumbu umbali wa km 38.

Alisema,mahitaji ya shule ya sekondari kwa wavulana na wasichana wa kata hiyo wanaomaliza darasa la saba yalikuwa makubwa, kwa hiyo kama wadau wakaona  kuna umuhimu wa kuunga mkono kwa kujenga madarasa hayo.

Linus ambaye ni Mchungaji wa Kanisa la Anglikana Doyasisi ya Masasi,ameshukuru  mashirika hayo yenye makao makuu yake  nchini Uingereza na Ubelgiji  kuweza kukamilisha ndoto za vijana wengi wa kata hiyo hasa wa kike ambao ndiyo  hasa waliongoza kukatisha masomo yao kwa sababu ya kutembea umbali mrefu kutoka katika vijiji vyao kwenda kwenye shule walizopangiwa kuendelea na elimu ya sekondari.

Alisema,kama wadau wa maendeleo wataendelea kushirikiana na serikali kutatua baadhi ya changamoto katika sekta ya elimu,maji,afya na zile zilizopo katika  vijiji kwa kukaa na  jamii ili kuibua miradi itakayowezesha kupata fedha kutoka kwa wafadhili.

Ameipongeza serikali kwa kuwekeza nguvu kubwa katika ujenzi wa miundombinu katika sekta ya elimu hapa nchini,na kuwaomba wadau  mbalimbali kuungo mkono juhudi hizo ili vijana wengi wanaomaliza darasa la saba wapate nafasi ya kuendelea na elimu ya sekondari.

Mwakilishi wa Eucanaid kutoka Ubelgiji Edgar Thielinann alisema, kijiji hicho ni muhimu sana kwao kwa kuwa elimu ni moja ya kipaumbele kikubwa na wamefurahi kuona shule hiyo imeshafunguliwa,ina wanafunzi,walimu na vifaa vya kufundishia.

Alisema,huo ni mwanzo tu na wanajua bado kuna  changamoto nyingi kwa kuwa kuna wanafunzi wengine watakuja kusoma katika shule hiyo na kuomba ushirikiano ulioonyeshwa kati ya wananchi,serikali na shirika hilo  uendelee.

Kwa upande wake David Gibbons kutoka  shirika la TDT la Uingereza alisema,mwaka 2019 alipotembelea kijiji cha Marumba kwa ajili ya kutembelea miradi inayotekelezwa na shirika hilo alipata nafasi ya kufika shule ya Mkanona ambayo majengo yake yalikuwa machache na porini.

Alisema,akiwa na Linus Buriani mwakilishi wa TDT Nchini Tanzania, walijadiliana sana juu ya kuisaidia shule hiyo ili  kuongeza idadi ya majengo  kwa ajili ya wanafunzi na walimu waliopangiwa kufanya kazi katika shule hiyo.

Hata hivyo,ameshukuru kuona  baada ya kurudi Uingereza alipata picha za  baadhi ya wananchi wakishiriki katika ujenzi wa shule hiyo kwa kuchimba mitaro,kubeba mawe na wengine kushiriki katika ujenzi ambapo alivutiwa na jitihada hizo za wananchi wa Namijati na kuamua kutafuta wafadhili wengine watakoungana na TDT ili kuongeza idadi ya majengo  na miundombinu mingine ya shule.

Mkuu wa wilaya ya Nanyumbu Mariam Chaurembo,amewashukuru wafadhili shirika la Tanzania Development Trust(TDT) na  Eucanaid kusaidia kutatua changamoto  katika maeneo mbalimbali wilayani humo.

Alisema,kabla ya kujengwa kwa shule hiyo wanafunzi wanaotoka kata ya Mkanona walilazimika kutembea umbali wa km 38 kwenda shule ya Sekondari kata ya Nanyumbu jambo lililo sababisha baadhi yao kukatisha masomo.

Alisema,kuwepo kwa shule hiyo sasa kumesaidia kupunguza tatizo la kutembea umbali kufuata masomo,utoro  na kuongeza taaluma kwa wanafunzi.

Kwa mujibu wa mkuu wa wilaya,serikali ya awamu ya sita ilishajenga vyumba vinne vya madarasa kupitia fedha za mpango wa  maendeleo na mapambano dhidi ya Covid-19 na itaendelea kufanya hivyo kadri fedha zitakapopatikana.

Amewataka,wazazi,walezi na jamii kwa ujumla kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwamo ujenzi wa  miundombinu ya elimu,badala ya kazi hiyo kuiachia serikali peke yake.

Aidha alisema,serikali katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 itahakikisha inapeleka nishati ya umeme katika shule hiyo ili wanafunzi  waweze kusoma hata majira ya siku na walimu wafanye kazi zao wakati wote.

Chaurembo,amewaomba wafadhili hao kusaidia kuboresha(kupeleka) huduma ya maji  katika  shule hiyo na maeneo mengine  ya wilaya ya Nanyumbu ili kupunguza na kumaliza kero ya wanafunzi na jamii kutembea umbali mrefu kutafuta maji safi na salama kwa matumizi ya kila siku.

Mbunge wa Jimbo la Nanyumbu Ali Yahaya alisema, ujenzi wa shule hiyo ni hatua kubwa ya kimaendeleo katika jimbo  la Nanyumbu kwa kuwa itasaidia vijana wa kata ya Mkanona wanaochaguliwa kuanza kidato cha kwanza kuendelea na elimu ya sekondari.

Amewaomba wafadhili na wadau wengine,kuangalia uwezekano wa kujenga mabweni ili wanafunzi wote waishi shuleni badala ya kutokea nyumbani na nyumba za walimu ili kuepuka kupanga uraiani ambapo wananchi wako tayari kushiriki na kujitolea nguvu zao.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.