• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TAKUKURU Ruvuma yaokoa zaidi ya milioni 100

Imewekwa kuanzia tarehe: April 30th, 2021

Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Ruvuma imeokoa kiasi cha fedha Shilingi Milioni 102,968,122/= ambazo zimepatikana baada ya chunguzi mbalimbali kufanyika.

Taarifa hiyo imetolewa na Kaimu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Owen Jasson, wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi wa TAKUKURU kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Marchi 2021 kwa Waandishi wa Habari iliyofanyika  katika ofisi za TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma tarehe 28 Aprili 2021.

Jasson alisema katika kipindi cha miezi mitatu, Taasisi hiyo imefanikiwa kuokoa fedha kiasi cha jumla ya Shilingi Milioni 102,968,122/= ambayo imeokolewa kutokana na chunguzi zilizofanyika kwenye vyama vya ushirika (SACCOS)  Wilaya ya Songea, Mbinga, Namtumbo, Tunduru na Nyasa.

Jasson alibainisha kuwa  fedha hizo zimetokana na marejesho ya madeni kutoka kwenye vyama mbalimbali vya ushirika katika mkoa wa Ruvuma ikiwemo na SACCOS ya walimu (Tunduru), Nambawala AMCOS (Nyasa), Kurugenzi SACCOS (Mbinga), SACCOS (Songea) pamoja na Libango AMCOS (Namtumbo).

Aliongeza kuwa katika kipindi hicho tajwa, Taasisi hiyo imefuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo 13 Mkoa wa Ruvuma ambayo ni ujenzi wa miundo mbinu ya maji, barabara, elimu na huduma za vikundi, inayotekelezwa katika Wilaya zote Mkoani Ruvuma  yenye thamani Zaidi ya Shilingi Bilioni moja ikiwemo mradi wa ujenzi wa nyumba 7 za watumishi wa Wilaya ya Madaba.

Aliongeza kuwa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma imefanikiwa kufanya semina na mikutano ya hadhara sehemu mbalimbali kwa ajili ya  kutoa elimu kwa jamii juu ya mapambano dhidi ya Rushwa, na kuimarisha klabu za wapinga Rushwa katika shule za msingi na sekondari, Jasson ‘Alisema’.

Aidha, amewashukuru Wananchi kwa kusaidia Taasisi hiyo katika kutoa taarifa kuhusiana na vitendo vya Rushwa kupitia vyanzo mbalimbali ambapo wamefanikisha kupokelewa kwa taarifa 133 katika kipindi hicho cha Januari hadi Marchi 2021.

TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma imejipanga kuendelea kuelimisha jamii kupiga vita Rushwa kwa kuwafahamisha madhara ya kutoa na kupokea Rushwa, kutoa taarifa mapema juu ya vitendo vya Rushwa, kuwa tayari kutoa ushahidi pale inapohitajika pamoja na kuendelea kufuatilia miradi ya maendeleo linayoendelea kutekelezwa katika kipindi cha Aprili hadi Juni 2021.

IMEANDALIWA NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA,

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.