• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TAMCU yaingiza zaidi ya bilioni 300 kwenye korosho,RC Ibuge apongeza

Imewekwa kuanzia tarehe: August 8th, 2021

CHAMA kikuu cha Ushirika katika wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma(TAMCU LTD) kimeuza jumla ya  kilo milioni  106,813,115 ya zao la korosho zenye thamani ya Sh bilioni 310,336,306,090.0 katika kipindi cha miaka minne.

Meneja Mkuu wa Tamcu Imani Kalembo amesema hayo,wakati akitoa taarifa ya hali ya uzalishaji wa zao hilo  kwa Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Brigadia Jenerali Wilbert Ibuge.

Katika msimu wa kilimo 2016/2017 Chama hicho kimeuza  kilo 15,189,913 zenye thamani ya Sh 46,899,462,396.00,mwaka 2017/2018 kimeuza kilo 20,912,569 zenye thamani ya Sh 79,777,589,485.00,mwaka 2018/2019 kilo 18,586,248 zenye thamani ya Sh 61,334,618,400.00.

Kwa mujibu wa Kalembo,mwaka 2019/2020 kilo 24,625,824 zenye thamani ya Sh 65,376,990,905.00 na katika msimu wa 2020/2021 jumla ya kilo 15,410,551 zenye thamani ya Sh 33,088,547,389.00. zimeuzwa.

Aidha, Tamcu kupitia vyama vya msingi kimekusanya na kuuza jumla ya kilo  9,881,714 ya zao la ufuta lililowaingizia wakulima zaidi ya Sh 22,552,420,857.00 huku zao la mbaazi katika msimu wa 2020/2021 kilo zilizouzwa ni 2,206,296 zenye thamani ya Sh 1,306,676,658.00.

Kalembo amesema kuwa, mauzo hayo yamefanyika kwa kutumia mfumo wa stakabadhi ghalani mfumo ambao wanachama(wakulima) wameukabali kwa kuwa umeleta tija kubwa kwao ikiwemo bei nzuri ya  mazao hayo.

Amesema,katika kipindi  cha miaka minne  iliyopita,Chama Kikuu cha Ushirika Tamcu kimesimamia upatikanaji wa Pembejeo na kutoa mikopo kwa wanachama yenye thamani ya Sh Bilioni 1,670,584,000.00.

Amesema kuwa, mikopo hiyo imewasaidia sana wanachama kuongeza uzalishaji wa korosho kutoka kilo 15,301,037 mwaka 2017 hadi kufikia kilo 24,625,824 mwaka 2019/2020.

Katika hatua nyingine Kalembo ameeleza kuwa,kupitia Vyama vikuu vya Ushirika hadi kufikia tarehe 24 Julai wameshapokea Viuatilifu  vya maji na unga kwa ajili ya kupulizia mikorosho.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Brigadia Jenerali Wilbert Ibuge amekipongeza Chama hicho kwa kuwa na mikakati mizuri ya kuwasaidia wakulima na kuimarisha zao la Korosho.

Amesema, Serikali haiwezi kutoa Viuatilifu vinavyokidhi kwa kila mmoja kwa muda wote,hivyo ni lazima kuwa na sehemu ya kujazia(kuongeza)  mkulima mwenyewe kwa kulima mazao mengine yatakayomuingizia kipato wakati anasubiri msimu wa zao la korosho.

Hata hivyo,ameagiza suala la elimu ya kilimo bora na chenye tija  kwa wakulima na kuendelea kuhamasisha wakulima kulima mazao mengine ya biashara kama  kama Soya,Alizeti ambayo yatawasaidia kuongeza kipato.

Amesema, serikali itaendelea kutafuta masoko ili kuwezesha mkulima kuwa na uhakika wa kuendelea kuzalisha na kupitia vyama vya msingi waweze kupata elimu hasa  kwa mazao mapya yatakayolimwa na kuuza kwa mfumo wa  stakabadhi ghalani na kukomesha kuuza  kupitia vipimo haramu vya kangomba.

MWISHO.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.