• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TANESCO inavyoyaangza maisha ya wananchi vijijini

Imewekwa kuanzia tarehe: February 23rd, 2025

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoani Ruvuma limeendelea na kampeni yake ya kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi sahihi ya umeme, utunzaji wa miundombinu, na utaratibu wa kuomba huduma hiyo muhimu. Kampeni hii inatekelezwa katika maeneo mbalimbali, ikiwemo kijiji cha Mkurumusi, Kata ya Mpitimbi.


Katika ziara hiyo, wananchi walipatiwa mafunzo kuhusu njia bora za kutunza miundombinu ya umeme na kujiepusha na vitendo vya hujuma kama wizi wa mafuta ya transfoma na nyaya za umeme aina ya kopa. Aidha, walipewa maelekezo ya jinsi ya kuomba umeme kwa njia za kidigitali kwa kutumia simu janja ili kurahisisha upatikanaji wa huduma.


Afisa Habari na Uhusiano wa TANESCO Ruvuma, Allan Njiro, alisisitiza kuwa kabla ya kuomba umeme, ni lazima nyumba ziwe na wiring sahihi na ziwe ndani ya maeneo yenye nguzo zinazofikika. Alieleza kuwa gharama ya kupata umeme kwa wakazi wa vijijini ni shilingi 27,000 kwa njia moja, huku gharama ya njia tatu kwa matumizi ya viwanda ikiwa shilingi 139,000, na wakazi wa mijini wakitakiwa kulipia shilingi 321,000.


Kaimu Afisa Habari na Huduma kwa Wateja, Emma Ulendo, alieleza kuwa umeme ni msingi wa maendeleo ya kijamii na kiuchumi, hivyo ni muhimu wananchi kuhakikisha wanakamilisha taratibu zote muhimu ili kupata huduma hiyo kwa urahisi. Pia, alibainisha kuwa serikali na TANESCO wanaendelea na mpango wa kuhakikisha kila mwananchi, hata walio nje ya kilomita 30, wanapata umeme kwa gharama nafuu.


Mwenyekiti wa kijiji cha Mkurumusi, Casian Joseph Kayombo, akiwasilisha maombi kwa niaba ya Diwani wa Kata ya Mpitimbi, Mheshimiwa Issa Kindamba, aliiomba TANESCO kuwaharakishia wakazi wa eneo hilo huduma ya umeme. Pia, aliipongeza serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan na Mbunge wa Songea Vijijini, Mheshimiwa Jenista Mhagama, kwa juhudi zao katika kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa uhakika.


Wananchi wa Mpitimbi wamepokea kwa furaha taarifa za kuletwa kwa umeme katika maeneo yao na wameahidi kushirikiana na TANESCO kulinda miundombinu. Aidha, wameomba serikali kuharakisha utekelezaji wa mradi ili kuhakikisha kila kaya inanufaika na huduma hiyo muhimu kwa maendeleo yao.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru 2025 waikubali miradi yote Mbinga

    May 12, 2025
  • WANANCHI walivyojitokeza kuupokea mwenge wa Uhuru katika kijiji cha Maguu Mbinga

    May 11, 2025
  • MAHABA ya wananchi wa Mbuji wilayani Mbinga kwa Mwenge wa Uhuru 2025

    May 11, 2025
  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.