• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TANGAWIZI yawaingizia wakulima Madaba zaidi ya bililioni moja

Imewekwa kuanzia tarehe: December 8th, 2020


WAKULIMA wa Halmashauri ya Madaba wilayani Songea mkoani Ruvuma wamepata zaidi ya shilingi bilioni moja kutokana na mauzo ya zao la tangawizi katika kipindi cha mwaka 2019/2020.

Afisa Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika wa Halmashauri hiyo Joseph Mrimi akizungumza ofisini kwake mjini Madaba,amesema kutokana na mauzo hayo  Halmashauri imeingiza zaidi ya shilingi milioni 16 ambazo ni mapato ya ushuru sawa na asilimia tatu ya mapato .

Mrimi amesema uzalishaji wa tangawizi katika Halmashauri hiyo msimu huu umefikia tani 5,117 ambazo zimeuzwa  ndani na nje ya Nchi.

“Halmashauri ya Wilaya ya Madaba tumeweka mkakati wa kuongeza  thamani ya zao hilo na kuongeza uzalishaji zaidi wa zao hilo ambalo soko lake hivi sasa ni kubwa’’,alisisitiza Mrilimi.

Amesema Halmashauri imetenga jumla ya Hekari 400 kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda mbalimbali vya kuchakata mazao ya kilimo ikiwemo zao la tangawizi.

Kwa upande wake Mchumi wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Bosko Mwingira amesema,Halmashauri ya Wilaya hiyo imechukua hatua mbalimbali za kulitangaza zao hilo  katika maonesho ya wakulima nanenane Kanda ya Mbeya na Maonesho  ya Uwekezaji katika Mkoa wa Ruvuma.

Amesema tayari Kampuni ya TANZANICE imeahidi kununua tangawizi toka kwa wakulima wa Madaba ,na kwamba matarajio ya Halmashauri siku zijazo ni kupata msindikaji mkubwa.

Hata hivyo amesema Halmashauri imejipanga kuwahamasisha wakulima  wanaoweza kulima na kusindika zao hilo ambapo amejitokeza Mkulima mmoja toka Kijiji cha Ifinga kulima na kusindika zao hilo.

Amesema ni azma ya Halmashauri hiyo kwa kushirikiana na  wadau mbalimbali kununua na kusindika tangawizi  ili zao hilo liendelee kuongeza uchumi wa Madaba na Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa Habari Halmashauri ya Madaba

Desemba 7,2020

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.