• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TANGAZO muhimu la kujiandikisha kupiga kura mkoani Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: October 3rd, 2024

wananchi wa Mkoa wa Ruvuma mnatangaziwa kuwa Uandikishaji wa wapiga kura utafanyika kwa muda wa siku kumi kuanzia tarehe 11 Oktoba, 2024 hadi tarehe 20 Oktoba 2024.

➢ Kwa upande wa vijiji Uandikishaji utafanyika katika kitongoji kwa ajili yauchaguzi wa mwenyekiti wa kijiji, wajumbe wa Halmashauri ya kijiji na mwenyekiti wa kitongoji.

➢ Kwa upande wa mitaa uandikishaji utafanyika katika mtaa kwa ajili ya uchaguzi wa mwenyekiti wa mtaa na wajumbe wa Kamati ya Mtaa.

 

Ndugu wananchi ,Uandikishaji wa wapiga kura utafanyika kwenye majengo ya umma na pale ambapo hakuna jengo la umma, uandikishaji utafanyika sehemu ambayo Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi atakuwa amekubaliana na viongozi wa vyama vya siasa.

 

   Ndugu wananchi ,Vituo vya uandikishaji wa wapiga kura vitafunguliwa saa mbili kamili asubuhi na kufungwa saa kumi na mbili kamili jioni.

➢ Vyama vya Siasa vitaruhusiwa kuwekamawakala wao wakati wa uandikishaji wa wapiga kura kwa gharama zao.

➢ Wakati wa uandikishaji wananchi hawataulizwa masuala yanayohusu shughuli zao, uanachama wa chama cha siasa au dini.

 

 Ndugu wananchi,Tarehe 21 Oktoba, 2024 Orodha ya wapiga kura itabandikwa katika vituo vya kujiandikisha na kupiga kura ili kuwezesha wananchi kukagua orodha ya wapiga Kura.

➢ Mkazi aliyejiandikisha kupiga kura atakuwa na haki ya kuweka pingamizi katika muda wa siku saba kuanzia tarehe 21 Oktoba, 2024 hadi tarehe 27 Oktoba,2024.

Ndugu wananchi , Mpiga Kura atatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:

(a) ni raia wa Tanzania;

(b) ana umri wa miaka 18 au zaidi;

(c) ni mkazi wa kijiji au kitongoji au mtaa ambao Uchaguzi unafanyika;

(d) ana akili timamu; na

(e) awe amejiandikisha kupiga kura katika kitongoji au mtaa au kijiji husika.

        Ndugu wananchi .Mpiga kuraatapoteza sifa ya kupiga kura endapo:

(a) hana moja wapo ya sifa zilizoainishwa hapo juu;

(b) Amejiandikisha kupiga kura katika kituo zaidi ya kimoja.

     Sifa za Mgombea

➢ Mkazi yeyote wa kijiji au kitongoji au mtaa anaweza kugombea nafasi yoyote katika Uchaguzi endapo:

➢ ni raia wa Tanzania;

➢ ana umri wa miaka 21 au zaidi;

➢ anaweza kusoma na kuandika Kiswahili au Kiingereza;

➢ ana shughuli halali ya kumwezesha kuendesha maisha;

➢ ni mwanachama wa chama cha siasa na amedhaminiwa na chama hicho; na

➢ ana akili timamu.

 

Ndugu wananchi ,Mtu hatakuwa na sifa za kugombea nafasi yoyote katika uchaguziendapo: 

➢ amepoteza sifa zilizoainishwa hapo juu

➢ amehukumiwa hukumu ya kifo na Mahakama za Tanzania au anatumikia kifungo cha zaidi ya miezi sita gerezani;

➢ hajatangaza kuwepo kwa mkataba au maslahi katika kampuni yenye mkataba na kijiji ambacho anataka kugombea;

➢ amepoteza sifa ya kupiga kura; au

➢ ataajiriwa au kuteuliwa katika wadhifa wowote katika Utumishi wa Umma au kuchaguliwa katika nafasi ya udiwani, ubunge, uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

TANGAZO HILI LIMETOLEWA NA OFISI YA MKUU WA MKOA WA RUVUMA

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.