• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TANI 1,271 za kahawa zazalishwa na AMCOS Mbinga

Imewekwa kuanzia tarehe: April 16th, 2025

 Zaidi ya tani 1,271 za kahawa zimezalishwa na kukusanywa kupitia Chama cha Msingi cha Ushirika cha Liyombo Amcos katika msimu wa kilimo wa mwaka 2024/2025, huku wakulima wakinufaika kwa kupata kiasi cha Shilingi bilioni 10.96. Huu ni uzalishaji mkubwa zaidi kuwahi kufikiwa tangu kuanzishwa kwa chama hicho mwaka 2019.

Katibu wa Chama cha Liyombo Amcos, Angelina Nchimbi, alisema kuwa ongezeko hilo limekuja baada ya jitihada za pamoja kati ya chama na wakulima, ikilinganishwa na msimu wa 2023/2024 ambapo walizalisha tani 309 tu zenye thamani ya Shilingi bilioni 1.58. Alibainisha kuwa mfumo wa stakabadhi ghalani umeleta manufaa makubwa kwa wakulima na kusaidia kupata masoko yenye ushindani.

Mwenyekiti wa chama hicho, Joseph Mbele, alisema kuwa wamekuwa wakipata mikopo ya pembejeo kupitia Ofisi ya Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Ruvuma. Alifafanua kuwa msimu wa 2023/2024 walikopeshwa Shilingi milioni 180 na msimu wa 2024/2025 wameidhinishiwa mkopo wa Shilingi milioni 350, fedha zilizosaidia kununua mbolea, dawa na kulipia awamu ya kwanza ya malipo kwa wakulima.

Aidha, Mbele alisema kuwa kabla ya kuanzishwa kwa Amcos, wakulima walikuwa wakikumbwa na changamoto za kiuchumi kutokana na gharama kubwa za pembejeo na kukosa sehemu ya kuhifadhi kahawa, lakini kwa sasa wamepata mwelekeo mzuri kupitia chama hicho na ushirikiano na Bodi ya Ushirika ya Mbinga (Mbifacu).

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kitengo cha uzalishaji wa Amcos hiyo, Yukundus Hyera, alisema kuwa ruzuku ya pembejeo iliyotolewa na Serikali ya awamu ya sita imeboresha hali ya mashamba na kuongeza uzalishaji mara mbili zaidi. Alimpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha upatikanaji wa pembejeo kwa bei nafuu, hali ambayo imeleta mafanikio makubwa kwa wakulima wa kahawa wilayani Mbinga.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.