• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TANROADS kukamilisha barabara ya Amanimakoro-Ruanda

Imewekwa kuanzia tarehe: November 4th, 2024

WAKALA wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Ruvuma,umewahakikishia wakazi wa wilaya za Mbinga na Nyasa wanaotumia barabara ya Amanimakoro-Ruanda yenye urefu wa kilometa 35 kuwa,ujenzi wa barabara hiyo unaendelea na itakamilika mwaka 2025.


Kauli hiyo imetolewa na Meneja wa TANROADS Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Saleh Juma, baada ya kukagua ujenzi wa barabara hiyo inayojengwa kwa kiwango cha lami na Mkandarasi kampuni ya China Railway Sevent Group(CRSG) kwa gharama ya Sh.bilioni 60.4.


Amesema,barabara ya Amanimakoro-Ruanda ni ya kimkakati na muhimu kwa uchumi wa mkoa wa Ruvuma na Taifa kwa ujumla kwani inaunganisha wilaya ya Mbinga,Nyasa na mkoa jirani wa Njombe na inatumika kusafirisha makaa ya mawe kutoka Ruvuma kupeleka mikoa mbalimbali nchini na nje ya nchi.

Kwa mujibu wa Saleh kwa sasa kazi ya ujenzi inaendelea vizuri na kwamba matarajio ya Serikali barabara hiyo itakamilika haraka ili wananchi waweze kuitumia kwenye shughuli zao za usafiri na usafishaji.

Amesema,barabara hiyo ni sehemu ya barabara ya Kitai-Ruanda hadi Lituhi kuelekea Mbambabay wilayani Nyasa kupitia Bandari ya Ndumbi,ambapo Serikali iko katika maandalizi ya kujenga kipande kingine kutoka Ruanda hadi Lituhi kwa kiwango cha lami.

“kimsingi kazi inayofanywa na mkandarasi ni kuandaa lea ya kwanza na pili kabla ya kuweka lami,mpango wetu kwa mwaka huu 2024 tuwe na lami yenye urefu wa angalau kilometa tano,nachukua nafasi hii kuwaeleza wananchi wa mkoa wa Ruvuma kwamba, Mkandarasi yuko saiti na kazi inaendelea"alisema Saleh.


Amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa fedha zilizowezesha ujenzi wa barabara hiyo kuendelea na kuhaidi kumsimamia mkandarasi ili aweze kukamilisha ujenzi kazi kwa wakati kwani kuwa barabara hiyo inategemewa sana kuharakisha maendeleo na uchumi wa mkoa wa Ruvuma.

Msimamizi wa kitengo cha ndani kutoka TANROADS Mkoa wa Ruvuma Andrew Sanga amesema,mradi huo unahusisha ujenzi wa madaraja makubwa manne kati ya madaraja hayo, matatu ujenzi wake unaendelea ambapo moja limekamilika.
Kwa mujibu wa Sanga,ujenzi wa daraja la pili uko hatua za mwisho na mkanadarasi anamalizia kufunga nondo kabla ya kumwaga zege juu,na mategemeo ya wakala kwamba ujenzi wa madaraja yote yatakamilika kwa wakati.


Meneja mradi wa Kampuni yaCRSG amesema,kazi ya kipande cha barabara chenye urefu wa kilometa tano inaendelea vizuri na itakamilika ifikao mwezi Fabruari mwakani.

Baadhi ya wananchi,wameipongeza Serikali ya awamu ya sita kuendelea na ujenzi wa barabara hiyo ambayo inakwenda kufungua fursa mbalimbali za kiuchumi na kurahisisha usafiri kati ya vijiji vya kata ya Amanimakoro na maeneo mengine ya wilaya ya Mbinga na mkoa wa Ruvuma.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.