• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TANROADS RUVUMA waanza matengenezo makubwa barabara ya Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: August 17th, 2022

WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) mkoa wa Ruvuma, imeanza kufanya matengenezo makubwa katika barabara  zake zilizoharibika kutokana na mvua za masika na shughuli nyingine za kibinadamu katika maeneo mbalimbali.

Hayo yamesemwa na msimamizi wa mradi wa matengenezo ya barabaraya Songea-Tunduru Mhandisi Godfrey Robbi wakati akikagua kazi ya matengenezo ya barabara hiyo eneo la Mingwea wilayani Namtumbo.

Robi alisema,wameanza kufanya matengenezo ya barabara hiyo katika maeneo yote korofi kabla ya mvua za masika ili kuruhusu  barabara hiyo kuendelea kutumika kama kawaida katika shughuli mbalimbali za usafirishaji na uchumi.

Alisema, katika barabara hiyo inayounganisha mikoa ya Mtwara-Lindi na Dar es slaam baadhi ya maeneo yake yameharibika  kutokana na sababu mbalimbali na Tanroads inafanya matengenezo ili kuhakikisha hakuna shughuli za kiuchumi zinazosimama.

Mhandisi Robbi, ameyataja maeneo yaliyoanza kufanyiwa matengenezo ni Mingwea  kwa kurudisha tabaka la lami na eneo la Kaleo kwa kufikia korongo kubwa lililoanza kutishia usalama wa barabara.

Alisema,tatizo la kuharibika kwa barabara hiyo kumetokana na aina ya udongo na maji yanayopita chini ya  barabara kutokana na mvua zilizonyesha kwa wingi katika maeneo hayo korofi.

Amewatoa hofu wananchi  hasa watumiaji wa barabara hiyo,kuwa na matumaini kwa kuwa mkandarasi yupo eneo la mradi anaendelea na kazi ya kurudisha maeneo hayo katika hali yake ya kawaida.

Alisema, kazi ya matengenezo ya barabara hiyo itakamilika ifikapo mwishoni mwa mwezi huu wa Julai au mwanzoni mwa mwezi Agosti, kabla ya kuendelea na matengenezo ya barabara kongwe ya Songea-Njombe ambayo imeshachakaa kutokana na kujengwa kwa muda mrefu.

Kwa upande wake mwakilishi wa kampuni ya OVANS CONSTRUCTIONS LTD inayofanya matengenezo ya barabara hiyo  Mhandisi Azimio Mwapongo alisema, changamoto kubwa katika baadhi ya maeneo ya barabara  hiyo ni kuwepo kwa maji mengi chini ya ardhi.

Alisema baada ya kubaini tatizo hilo,  katika matengenezo ya sasa wameweka mfumo maalum chini ya ardhi ambao hauruhusu maji kukaa, na barabara hiyo itaweza kudumu kwa muda mrefu bila kufanywa matengenezo yoyote .

Ameongeza  kuwa,kutokana na matengenezo yanayofanyika ana uhakika tatizo  hilo halitarudia tena kwa kuwa kampuni ya Ovans Construction Ltd ina uzoefu mkubwa na wa muda mrefu katika miradi ya ujenzi wa barabara za lami hapa nchini.



Aidha,ameiomba Serikali kupitia TANROADS kujenga mizani kipande cha barabara ya Namtumbo  hadi Tunduru ili kudhibiti uzito wa magari yanayopita katika barabara hiyo kwa kuwa madereva wana tabia ya kuongeza mizigo mara baada ya kupitia mizani ya Songea.


Mmoja wa madereva wa magari makubwa  Denis Mbawala, ameishukuru Tanroads mkoa wa Ruvuma kwa uamuzi wa kufanya matengenezo makubwa hayo na kuipongeza kampuni ya Ovans Contructions Ltd kwa kazi nzuri  inayofanya katika matengenezo ya  barabara na miradi mbalimbali katika wa mkoa wa Ruvuma .


"kama mtumiaji wa barabara hii naishukuru Tanroads mkoa na Mkandarasi Kampuni ya Ovans kwa kazi nzuri inayofanya,nina uhakika matengenezo yanayofanyika hii barabara itaendelea kudumu kwa muda mrefu bila kufanyiwa matengenezo"alisema.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.