• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TANROADS waanza matengenezo ya Daraja Tunduru

Imewekwa kuanzia tarehe: March 6th, 2024

WAKALA wa barabara Tanzania(TANROADS) mkoa wa Ruvuma,imeanza kufanya matengenezo ya miundombinu ya barabara katika mto Namiungo wilayani Tunduru ambayo iliharibiwa na mvua na kutishia kukata mawasiliano kati ya mkoa wa Ruvuma na mikoa mingine ya Lindi,Mtwara,Pwani na Dar es slaam.

Msimamizi wa matengenezo kutoka Tanroads mkoani humo Mhandisi Godfrey Robbi alisema,tarehe 29 Februari mwaka huu mvua kubwa iliyonyesha kwa zaidi ya saa tatu ilisababisha maji kuvuka juu ya daraja na kupelekea upande mmoja wa daraja hilo kukatika na miundombinu yake kusombwa na maji.

Alisema,kutokana na umuhimu wa barabara hiyo kiuchumi hasa usafirishaji wa makaa ya mawe,wamelazimika kufanya matengenezo ya haraka ili kuruhusu shughuli za usafiri,usafirishaji na kiuchumi ziweze kuendelea kama kawaida.

Aidha alisema,wanaendelea kufanya matengenezo madogo kwenye maeneo mengine ya barabara hiyo ikiwemo eneo la Matemanga-Ligunga na Majala ambayo imeharibika vibaya ili kuwezesha watumiaji wake kupita kwa urahisi.

Robbi,amewataka wananchi hasa madereva kuzingatia alama zilizowekwa katika eneo hilo ili kuepusha madhara yanayoweza kutokea na wananchi kuacha ya kufanya shughuli za kibidamu ikiwemo kilimo ndani ya hifadhi ya barabara, kwani wanaweza kupata hasara pindi maeneo hayo yanapohitaji kupitisha vifaa vinavyotumika kwenye matengenezo ya barabara.

Naye Mhandisi wa kampuni ya Ovans Contructions Ltd inayofanya matengenezo ya daraja hilo Azimio Mwapongo alisema, kazi inayofanyika katika eneo hilo ni kurudisha miundombinu yote iliyosombwa na maji.

Alisema,wameanza kujaza mawe kabla ya kumwaga zege ili kuunganisha zege na lami kwa ajili ya kuzuia maji kupenya kwenye tuta la barabara na kurekebisha baadhi ya alama nyingine zilizoharibika.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.