• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TANZANIA kuwekeza nishati jadidifu

Imewekwa kuanzia tarehe: September 7th, 2023

SHIRIKISHO la Taasisi Ndogo za Fedha Tanzania (TAMFI) limeingia makubaliano na Chama cha Nishati Jadidifu Tanzania (TAREA) kuona namna bora ya kuongeza kasi ya kuwekeza katika matumizi ya nishati jadidifu nchini Tanzania.

Uongozi wa pande hizo mbili wakizungumza katika kongamano la siku mbili kuhusu uwekezaji katika nishati jadidifu, wamesema kumekuwepo na ongezeko la matumizi ya nishati hiyo hivyo ni lazima hatua zichukuliwe kuhakikisha kwamba wananchi wanapatiwa uwezo wa kuipata na kutumia.

Katibu Mtendaji wa Tamfi, Winnie Terry, akizungumza alisema: "Nishati mbadala sio tu inatakiwa kwa siku zijazo; ni ya sasa. Ushirikiano wetu na Tarea ni ushahidi wa kujitolea kwetu kufanya nishati mbadala kupatikana kwa wote."

Naye Katibu Mtendaji wa Tarea, Dk Matthew Matimbwi alisema: “Kupanda kwa takwimu za kuunganishwa kwa nishati ya jua, inayofikia asilimia 30.4 ya umeme wa majumbani Tanzania, si takwimu tu, bali ni matumaini na maendeleo. 

“Makubaliano yetu na Tamfi yataongeza takwimu hizi na kuhakikisha mustakabali endelevu kwa Watanzania wote."

Tamfi na Tarea zimekubaliana kuhakikisha kuwa wajasiriamali chipukizi na wanajamii wanapata huduma sahihi za kifedha ili kuwezesha kupata nishati jadidifu.

Katika hatua kubwa ya kuziba pengo la ujuzi wa nishati ya jua, kituo cha mafunzo cha Don Bosco kinaendesha programu zinazolenga kupata mafundi wa nishati ya jua.

Alfred Dalasia - Ofisa Programu, Don Bosco, alisema katika kuimarisha sekta ya nishati mbadala wamewezesha mafunzo kwa vijana zaidi ya 1,000. 

Nayo Taasisi ya Nishati na Maisha kwa Jamii (E-LICO), imesema kama taifa juhudi lazima ifanyike juhudi kufikia kiwango cha juu cha matumizi ya nishati jadidifu kwa ajili ya kuinua kijamii vijijini Afrika.

“Tunasaidia kwa kukopesha vifaa vya nishati ya jua kwa wakulima, kuwasaidia katika kuchimba visima na kuendesha mifumo yao ya umwagiliaji. Mradi wetu wa sasa uko Iringa na Dodoma—shukrani kwa msaada wa wafadhili—lengo letu ni kupanua wigo wetu nchini Tanzania na labda hata Afrika,” alifafanua Tulibako Mwansasu kutoka Taasisi ya E-LICO.

Alisema lengo la E-LICO sio tu kuwasha taa nyumbani bali  ni kuendesha biashara za wakulima, wafugaji, na wavuvi. 

"Tunawapa zana za umeme na kuwaelimisha jinsi ya kuzitumia. Na kwa matatizo ya vifaa, tunawaunganisha na wahandisi wa ndani. Tunatoa pia suluhisho kama vile friji zinazoendeshwa kwa nishati ya jua, zinazosaidia kuhifadhi bidhaa muhimu kama samaki, nyama, na maziwa katika maeneo ambayo umeme ni vigumu kupatikana.” alisema.

Tanzania ina uwezo mkubwa wa nishati endelevu, na rasilimali nyingi za jua, upepo, maji, na jotoardhi. Serikali ya Tanzania imejiwekea lengo la kuzalisha 50% ya umeme wake kutoka vyanzo vya nishati endelevu ifikapo mwaka 2030.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DKT Nchimbi awaongozawananchi kuuaga mwili wa Mzee Songambele

    June 02, 2025
  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.