• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TANZANIA PROJECT yaikabidhi serikali sekondari mpya Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: March 14th, 2025

Serikali imepokea rasmi shule mpya ya sekondari Lovund iliyojengwa na Mradi wa Tanzania Project katika Wilaya ya Nyasa, mkoani Ruvuma.

Makabidhiano hayo yalifanyika katika viwanja vya shule hiyo, huku mgeni rasmi akiwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed, aliyewakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Nyasa, Mhe. Peres Magiri.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma alipongeza Mradi wa Tanzania Project kwa kujenga shule hiyo, akisema imeondoa changamoto ya wanafunzi kutembea zaidi ya kilometa saba kufuata elimu.

Alitoa wito kwa walimu, wazazi na wanafunzi kuitunza miundombinu ya shule ili kuwezesha utoaji wa elimu bora kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Mratibu wa Mradi huo, Mwl. Dennis Katumbi, alieleza kuwa ujenzi unatarajiwa kugharimu shilingi bilioni 1.2, ambapo hadi sasa shilingi milioni 998 zimetumika,.

Amesema utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 87 ya miundombinu ambapo serikali kuu imechangia shilingi milioni 20 kwa ajili ya kukamilisha bweni la wasichana.

Amesema awamu ya nne ya mradi inahusisha ujenzi wa maktaba, nyumba moja ya walimu, kichomea taka na uzio wa shule.

Mbunge wa Nyasa, Mhandisi Stella Manyanya, aliipongeza Tanzania Project kwa mchango wake katika sekta ya elimu na kuwataka wazazi kuhakikisha watoto wao wanatumia fursa hiyo ya elimu.

Mkurugenzi wa mradi huo, Hanne, aliwashukuru wafadhili kutoka Norway na kusisitiza kuwa elimu ni ufunguo wa maendeleo kwa jamii.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa aliahidi majengo hayo yatatunzwa ili elimu bora itolewe kwa wanafunzi.

Mwakilishi wa Ubalozi wa Norway aliahidi kuendeleza ushirikiano kati ya Tanzania na Norway kwa maendeleo ya sekta ya elimu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.