• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TANZANIA PROJECT yatoa msaada wa vifaa vya kupambana na corona Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: April 8th, 2020

Shirika lisilokuwa la Kiserikali la Tanzania Project, Wilaya ya Nyasa  limetoa msaada wa  vifaa vya kunawia maji  vyenye Thamani Ya Tsh 3,710,000/= kwa Wananchi wa Wilaya ya Nyasa  ili kujikinga na Virusi vya Corona .

Vifaa hivyo vimekabidhiwa leo na Mratibu wa Shirika hilo Wilayani Nyasa Denis Katumbi kwa Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Bi Isabela Chilumba ili, avigawe kwa wananchi wa Wilaya ya Nyasa ili wachukue tahadhari ya kukabiliana na Ugonjwa wa Corona kwa kunawa mikono .

Akikabidhi vifaa hivyo Bw. Katumbi alifafanua kuwa Shirika la Tanzania  project linawajali wananchi  wa Wilaya ya Nyasa na amepokea msaada huo kutoka makao makuu ya Shirika hilo yaliyopo Nchini Norway ili kuwasaidia na kuwawezesha watanzania walioko Nyasa kujikinga na kuchukua Tahadhari dhidi ya Ugonjwa Hatari wa Corona ambao hauna   dawa.

Alivitaja vifaa alivyochangia kuwa ni, Ndoo na mifuniko yake ya kunawia maji mia moja arobaini na nane (148) na sabuni za kunawia, za nusu  lita ,  mia tano sabini na mbili (572) na kutoa wito kwa wananchi wote wa Wilaya ya Nyasa kufuata maelekezo ya wataalamu wa Afya pamoja na Viongozi wa Serikali ili waweze kujikinga na Ugonjwa wa Corona.

Akipokea Msaada huo kwa niaba ya Wananchi wa Wilaya ya Nyasa,Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Bi Isabela Chilumba amelishukuru Shirika hilo kwa kutoa Msaada  kwa wananchi wa Wilaya ya Nyasa kwa kuwa ni Msaada ambao ulikuwa ukihitajika,lakini alisema shirika hilo limeonyesha ni jinsi gani linawapenda wananchi wa Wilaya ya Nyasa hivyo aliwataka wananchi wa Wilaya ya Nyasa kuhakikisha wanakuwa na sehemu nyingi za kunawa mikono, ili kujikinga na Ugonjwa wa Corona.Aidha alisema atagawa katika Taasisi zote na sehemu zenye mahitaji ya Vifaa hivyo.

“Nachukua fursa hii kuwapongeza sana ndugu zangu wa Tanzania Project Toka Nchini Norway kwa kujali Afya za wananchi wa Nyasa msaada waliotupatia ni mkubwa mno na ni wakati muafaka wa mapambano dhidi ya Corona hivyo tutahakikisha tunagawa katika masoko yote Wilayani hapa na kuhakikisha tunatoa elimu kwa wananchi wote wilayani hapa ili kupambana na Ugonjwa wa Corona”alisema Bi Chilumba.

Kwa kuanzia Leo amegawa vifaa hivyo katika Soko la Kilosa, Soko la Mbamba-bay na madereva wa Bodaboda wa Stand ya Mbamba-bay Wilayani hapa.

Imeandaliwa na

NETHO C.SICHALI

KAIMU AFISA HABARI

Nyasa dc 0767417597

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.