• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TARAFA ya Mpepo Nyasa inaongoza kwa kutoa chakula cha mchana kwa wanafunzi

Imewekwa kuanzia tarehe: August 29th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma Mheshimiwa Peres Magiri ameipongeza Tarafa ya Mpepo wilayani humo kwa kufanikiwa kutoa chakula cha mchana kwa shule zake zote.

Ametoa pongezi hizo wakati anazungumza kwenye kikao cha tathmini ya mkataba wa  lishe katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa katika kipindi cha kuanzia Aprili hadi Juni 2024 ambacho kimefanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Kilosa Mbambabay.

Amewaagiza watendaji wote wa Kata na wadau wa afya na lishe kusimamia utekelezaji wa shule zote kutoa chakula cha mchana kwa wanafunzi ili kupunguza udumavu unaoikabili  Wilaya ya Nyasa na Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla.

“Nawaagiza watendaji Kata wote katika wilaya ya Nyasa,kuhakikisha shule zote zinatoa chakula cha mchana kwa wanafunzi kwa sababu haya ni maamuzi yaliyopitishwa kwenye vikao vya vijiji na Kata’’,alisisitiza.

Sanjari na agizo hilo,Mkuu wa Wilaya pia ameagiza kila shule angalau iwe na bustani ya mboga ili kupata lishe bora kwa sababu,shule zinazotoa chakula cha mchana kwa wanafunzi sehemu kubwa , wanafunzi wanakula kande za mahindi yaliyokobolewa hivyo kukosa virutubisho muhimu na kusababisha udumavu kuendelea.

Taarifa ya tathmini ya Mkataba wa lishe katika Halmashauri ya Nyasa iliyotolewa katika kikao hicho,inaonesha kuwa katika kipindi cha kuanzia Aprili hadi Juni 2024 jumla ya wanafunzi 49,161 kati ya 58,191 wanapata angalau mlo mmoja wawapo shuleni  sawa na asilimia 84.48 .

Kulingana na taarifa hiyo katika kampeni iliyofanyika Mwezi Juni mwaka huu, Watoto 23,504 kati ya 23,504  sawa na asilimia  100 walipatiwa matone ya vitamini A.

Hata hivyo taarifa hiyo inaonesha kuwa katika kipindi hicho Watoto 15 kati ya 14,665 sawa na asilimia 0,001 waligundulika na utapiamlo mkali na kwamba wote walipatiwa matibabu.

Ili kukabiliana na utapiamlo na udumavu wilayani Nyasa,baadhi ya mapendekezo yaliyotolewa kwenye kikao hicho ni Pamoja na shule zote za msingi na sekondari kulima bustani za mboga,matunda na kuendelea kuhamasisha wanafunzi shuleni kutumia unga ulioongezwa virutubisho.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.