• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TARURA Ruvuma yaingia mikataba 41 ya matengenezo ya barabara na madaraja

Imewekwa kuanzia tarehe: September 4th, 2023

TARURA Mkoa wa Ruvuma imeingia mikataba 41 ya matengenezo ya barabara na ujenzi wa madaraja na makalavati inayogharimu zaidi ya shilingi bilioni 11 katika mwaka wa fedha 2023/2024.

Meneja wa TARURA Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Wahabu Nyamzungu amesema mikataba hiyo inatekelezwa katika kipindi cha miezi sita kuanzia Septemba 2023 hadi Machi 2024.

Amesema Mkoa wa Ruvuma umetengewa bajeti ya  zaidi ya shilingi 22 kwa ajili ya matengenezo ya barabara katika Halmashauri zote za Mkoa wa Ruvuma.

Kulingana na Meneja huyo wa Mkoa, Manispaa ya Songea imepangiwa kilometa 513.65, Wilaya ya Songea kilometa 1057.24, Halmashari ya Madaba kilometa 629.69,Wilaya ya Namtumbo kilometa 975.25,  Mbinga mji kilometa 1063.51,Mbinga vijijini kilometa 973.340, Wilaya ya Nyasa  kilometa 729.91 na Tunduru kilometa 1203.61.

Hata hivyo amesema Miradi mbalimbali ya barabara iliyotekelezwa mwaka wa fedha wa 2022/2023 na inaendelea kufanyiwa ukarabati  katika mwaka wa fedha 2023/2024.

“Natoa wito kwa wakandarasi ambao wanaenda kutekeleza kazi za ujenzi wa miundombinu ya barabara kwa mwaka 2023/224 kufanya kazi kadri ya mikataba inavyoelekeza na kumaliza kazi kwa wakati’’,alisisitiza Nyamzungu.

Amezitaja baadhi  changamoto zinazowakabili kuwa ni magari yenye uzito mkubwa kupita kwenye barabara zilizo chini ya wakala na kusababisha uharibifu mkubwa wa barabara na miundmbinu yake.

Changamoto nyingine ameitaja kuwa ni wananchi kuendesha shughuli za kilimo katika maeneo ya hifadhi ya barabara pamoja na kupitisha mifugo yao.

Ili kukabiliana na changamoto hizo amesema, TARURA ina mpango wa kuanzisha utaratibu wa kupima uzito wa magari katika barabara zake na kampeni maalum za ukamataji wa magari yanayozidisha uzito na ujazo ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.