• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TARURA yaanza kujenga barabara za mitaa kiwango cha lami Mbambabay

Imewekwa kuanzia tarehe: March 15th, 2023

WAKALA wa barabara za vijijini na mijini Tanzania(Tarura),imeanza ujenzi wa barabara za lami katika mitaa mbalimbali ya mji wa mdogo wa Mbambabay wilayani Nyasa unaotajwa kuwa mji pekee wa kitalii mkoani Ruvuma.

Meneja wa TARURA wilayani Nyasa Thomas Kitusi amesema,ujenzi wa barabara za lami ulianza mwaka wa fedha 2022/2023 kwa lengo la kuboresha na kupandisha adhi ya mji huo wenye vivutio vingi vya kitalii ikiwemo ziwa Nyasa na fukwe za kitalii zinazohitaji kuendelezwa.

Alisema,TARURA ilipokea jumla ya shilingi milioni 500 kutoka mfuko wa Jimbo  ambapo fedha hizo zimeleta mabadiliko makubwa,hasa ikizingatiwa sehemu kubwa ya barabara za mitaa katika mji huo zilikuwa za udongo.

Alisema kabla ya ujenzi wa barabara za lami, wananchi walipata shida ya kupita kwenye barabara za mitaa zenye tope na kusababisha kero na usumbufu mkubwa pindi wanapotaka kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

Kwa mujibu wa Kitusi,kero hiyo sasa imekwisha na wananchi wa Mbambabay wameanza kupita kwenye barabara nzuri zilizojengwa kwa lami zilizobadilisha muonekano wa mji huo mkongwe hapa nchini.

Kitusi,amewataka wananchi wa Mbambabay na maeneo mengine kulinda na kutunza barabara hizo na kuacha kutupa taka kwenye mifereji na kuwa walinzi wa miundombinu ikiwemo taa zilizofungwa ili ziweze kudumu kwa muda mrefu na waweze kuzitumia katika shughuli za maendeleo.

Alisema,ni wajibu  kila mmoja kuhakikisha anakuwa mlinzi wa miundombinu hiyo kwani  fedha zilizotumika katika ujenzi huo zinatokana na kodi zao ambazo zingeweza kupelekwa katika maeneo mengine hapa nchini.

Baadhi ya wananchi wa mji wa Mbambabay,wameishukuru serikali kwa kujenga barabara za lami ambazo zimesaidia kumaliza kero ya kutembea kwenye tope hasa wakati wa masika na kurahisisha mawasiliano.

Dotto Makungulu mkazi wa kijiji cha Ndengele alisema,kujengwa kwa barabara za lami katika mitaa mbalimbali ya mji huo,kumepandisha adhi ya mji wa Mbambabay na kuongeza thamani ya nyumba zao.

Agnes Chimatila,amewapongeza wataalam wa Tarura kwa kusimamia ujenzi wa barabara hizo ambazo zimesaidia kurahisisha mawasiliano katika mitaa mbalimbali za mji huo na kuiomba serikali kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya ujenzi wa barabara za lami katika maeneo mengine ambayo bado kuna changamoto kubwa ya miundombinu ya barabara za uhakika.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.