• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TASAF kuzifika kaya zaidi ya milioni 1.4 nchini

Imewekwa kuanzia tarehe: April 22nd, 2021

Mfuko wa kunusuru kaya masikini Nchini (TASAF) imepanga kuzifikia kaya masikini milioni 1.45 sawa naongezeko la kaya laki tatu kwa kipndi cha pili awamu ya tatu.

Hayo ameyasema Gerson Mboramallamia kwaniaba ya Mkurugenzi wa TASAF Nchini kwenye kikao cha kuwajengea uwezo viongozi,watendaji na wawezeshaji wa mpango wa kunusuru kaya masikini kipindi cha pili awamu ya tatu kilicho fanyika katika ukumbi wa SACCOS ya Walimu Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma.

Mboramallamia amesema azma ya Serikali kupitia  TASAF ni kupunguza umasikini wa kipato na kuongeza kipato kwenye kaya masikini kwa kutumia rasilimali zilizopo kwa kuboresha huduma za jamii kama vile huduma ya maji , afya, barabara na vivuko kwa walengwa kufanyakazi.

Amesema katika awamu ya kwanza ya utekelezaji TASAF imefanikiwa kupunguza umasikini wa kaya kwa asilimia 10 na umasikini uliokithiri kwa asilimia 12 kwa walengwa kufanya shughuli za kiuchumi za ufugaji,kilimo,uvuvi,biashara ndogondogo na ajira za muda mfupi.

Ameongeza kwa kusema TASAF kipindi cha awamu ya kwanza kiliwafikia walengwa kwa asilimia 70 na kipindi hiki cha pili awamu ya tatu kimepanga kukamilisha asilimia 30 iliyobaki na kufikisha asilimia miamoja ya walengwa wote Nchini iliwaweze kunufaika na mfuko huo kupitia ruzuku za aina nne ambazo mfuko umebanisha katika kukabiliana na tatizo la umasikini

Mboramallamia amezitaja aina za ruzuku zitakazo tolewa kuwa ni ruzuku ya msingi inayotolewa kwenye kaya iliyopo kwenye mpango,ruzuku ya kutimiza masharti inayotolewa kwa kaya yenye walengwa wanaotakiwa kutimiza  masharti ya elimu na afya ,ruzuku ya walemavu inayotolewa kwa walemavu na ruzuku ya Watoto inayotolewa kwa Watoto wanaoishi kwenye kaya masikini.  

Kwaupande wake Katibu Tawala wa Wilaya ya Songea Pendo Daniel ameomba TASAF makao mkuu kuwarejesha kwenye mpango wa kunusuru kaya masikini walengwa ambao waliondolewa kwenye mpango baada ya kufanyika kwa uhakiki wakuzitambua kaya zinazostahili kuwepo kwenye mpango.


“Nimefurahishwa sana na maboresho ya kipindi hiki cha pili awamu ya tatu kwakufanya uhakiki na kuwabaini walengwa hewa ambao hawakustahili kuwepo kwenye mpango”,amesema Mhe.Menas Komba

Mhe. Komba amesema TASAF licha ya kunusuru kaya masikini imesaidia sana kaya hizo kujiunga na mfuko wa bima ya afya iliyoboreshwa ambayo inamwezesha mlengwa na wategemezi wake watano kupata huduma za matibabu kwa gharama ya shilingi elfu 30,000 kwakipindi cha mwaka mmoja.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Songea Simoni Bulenganija amewataka watendaji ambao wameteuliwa kufanya zoezi la uhakiki awamu hii kwenda kufanya kazi hiyo kwa uadilifu mkubwa na kuzingatia kiapo walichoapa.

Bulenganija amesema katika eneo la usimamizi na ufuatiliaji amejipanga vema katika zoezi hilo ili kuhakikisha kazi ya kuibua kaya masikini zenyesifa linafanikiwa kama Serikali inavyokusudia kufanikisha mpango wake wa kunusuru kaya masikini na umasikini uliokithiri nchini.

Mratibu wa TASAF wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea  Hosana Ngunge amesema katika zoezi la utambuzi wa kaya masikini jumla ya wataalam tisa wameteuliwa kutekeleza kazi hiyo  katika Vijiji 24 ambavyo awali havikuwaepo katika mpango.

Halmashauri ya wilaya ya Songea inajumla ya kaya 2743,Vijiji 56 ambavyo vyote vinaingizwa kwenye mpango wa kunusuru kaya masikini wa kipindi cha pili awamu ya tatu.

Mpango wa TASAF kipindi cha pili awamu ya tatu kilizinduliwa na hayati Rais Dkt John Pombe Magufuli mwaka 2020 na mpango huo utakamilika mwaka 2023.

Imeandikwa na Jacquelen Clavery

Afisa Habari Songea

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.